Call Us: 423 661-4734 | Email: requests@comeandreason.com      
JE, NI UTII WA IMANI AU WA SHERIA?

JE, NI UTII WA IMANI AU WA SHERIA?

Wana wa Israeli walipokaribia mwisho wa miaka yao 40 ya kutangatanga jangwani na walipokuwa karibu kuingia Kanaani, Yoshua aliyekuwa akiwaongoza alipokea ujumbe ufuatao kutoka kwa Mungu:

Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda kulingana na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kulia, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako. (Yoshua 1:7).

Unaelewaje maagizo haya? Unaposikia mwito wa kutii sheria ya Mungu, nini huja akilini mwako? Je, unafikiria sheria ya Mungu kama sheria za kibinadamu — kanuni zinazowekwa ambazo Mungu huzisimamia na kutekeleza kwa adhabu? Au unafikiria sheria ambazo Muumba aliweka katika utendaji wa uhalisia — sheria za fizikia, mvuto (gravity) , afya, na sheria za maadili?

Je, unasikia mwito wa Mungu wa utii kama vile mwito wa daktari wa kuishi kwa afya (katika mwafaka na sheria za afya), au unasikia mwito wa Mungu wa utii kama onyo la askari polisi la kutokukimbiza gari kwa mwendo kasi?

Ni ukweli wa kusikitisha wa historia kwamba sehemu kubwa ya Ukristo imekubali uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi sawa tu na sheria za wanadamu—kanuni zilizobuniwa na kutekelezwa kwa adhabu. Lakini hebu tuchunguze utii unaotokana na sheria, kanuni, vitisho vya adhabu, na utekelezaji wa sheria—ukilinganisha na utii unaotokana na upendo, uaminifu, ambao pia hujulikana kama imani. Kisha tuchunguze jinsi upendo na uaminifu vinavyopandwa katika mioyo na akili na kupelekea utii.

 

UTII WA SHERIA

Fikiria umesimama chini ya msalaba wakati Yesu anasulubiwa. Unazungumza na Kayafa na viongozi wengine wa dini ya Kiyahudi wanaomdhihaki, kumtesa, na kumsulubisha Kristo. Unadhani wangetoa majibu gani kwa maswali yafuatayo?

  • Je, ni muhimu kuwa na utii wa agano kwa Mungu? “Kabisa!” naweza kuwasikia wakisema, “Tunaishi kwa ili kutii agano—sisi sote tumetahiriwa ipasavyo kama agano linavyoagiza.”
  • Je, ni muhimu kuitii sheria ya Mungu? “Bila shaka. Na kama hawa wahalifu hawatakufa upesi, tutamwomba Pilato aharakishe vifo vyao ili tuweze kuitunza Sabato kulingana na sheria.”
  • Je, ni muhimu kuitii sheria ambayo Musa mtumishi wa Mungu alitupa? “Bila shaka! Maisha yetu yote tunaishi tukilenga kutii sheria hiyo.”

Na kama tungewauliza, “Kwa nini mnamsulubisha huyu mtu?” naweza kuwasikia wakijibu:

“Naam, umeshatueleza wewe mwenyewe—lazima tuwe watiifu kwa agano, lazima tutii sheria ya Mungu, lazima tutii sheria ambazo Mungu alitupatia kupitia Musa—na huyu mtu anazivunja mara kwa mara. Musa alituagiza tumpige kwa mawe mzinzi, lakini huyu mtu aliwasamehe. Musa alitupa ruhusa ya kuwataliki wake zetu, lakini huyu mtu alisema tusifanye hivyo. Musa alitufundisha tusifanye kazi siku ya Sabato, lakini huyu mtu aliwaponya wagonjwa siku ya Sabato na wanafunzi wake walivuna punje siku ya Sabato. Musa alitufundisha kuosha kwa namna fulani kabla ya kula, lakini huyu mtu hakuwaelekeza wanafunzi wake wafanye hivyo. Musa alitufundisha kwamba sheria lazima zitekelezwe na kwamba uovu lazima uondolewe katika jamii, na ndicho tunachofanya kwa sababu sisi ni watoto wa Abrahamu na wa Mungu, na tumejitoa kwa uaminifu na utii wa agano.”

Utii wa sheria na utekelezaji wa sheria hauna uwezo wa kubadili mioyo na akili, wala kusimika upendo, uaminifu, urafiki, uaminifu wa kudumu, na kujitoa. Utii wa uongozi wa Kiyahudi uliomsulubisha Kristo ulikuwa aina iliyowafanya wawe maadui wa Mungu huku wakidai kuwa watoto wake na kufanya kazi yake.

Mtume Paulo anashughulikia mwelekeo huu wote wa kisheria usio sahihi kuhusu utii katika kitabu cha Warumi, na analinganisha utii unaotokana na sheria na utii unaotokana na imani au uaminifu. Anaanza kitabu cha Warumi kwa kusema:

Kupitia yeye na kwa ajili ya jina lake, tumepokea neema na utume ili kuwaita watu kutoka mataifa yote katika utii unaotokana na imani. (Warumi 1:5).

Imani au uaminifu si kitu kinachoweza kuamriwa, kutungwa kwa sheria, kuagizwa, au kupatikana kwa njia ya sheria na utekelezaji wake. Uaminifu hujengwa juu ya uaminifu halisi wa maisha, unaohitaji ushahidi, ambao lazima ueleweke na kuishiwa. Uaminifu hauwezi kuanzishwa kwa tangazo, madai, amri, maagizo, kanuni, na masharti, na utadhoofishwa na vitisho na adhabu. Jaribu kupata uaminifu wa mtu kwa kumtishia kumdhuru au kumwadhibu ikiwa hatakuamini—haiwezekani kabisa! Sheria zilizolazimishwa na utekelezaji wake haziwezi kuvutia mioyo na akili, na hatimaye, zitawageuza wale wanaotumia mbinu hizo kama njia ya kutafuta haki kuwa waasi.

Paulo, akielewa hili, baada ya kutufundisha kwamba anawaita watu kwenye utii unaotokana na imani, anatueleza msingi wa imani hiyo. Katika Warumi 1:20 anaandika:

Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, sifa zisizoonekana za Mungu—uwezo wake wa milele na asili yake ya uungu—zimeonekana wazi, zikieleweka kutokana na mambo yaliyoumbwa, hivyo watu hawana udhuru (NIV msisitizo wangu).

Imani yetu kwa Mungu haijengwi juu ya madai, maneno, au amri, bali juu ya uhalisia, ushahidi, na ukweli. Mungu ni Muumba, na sheria zake ndizo sheria zinazoongoza jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Paulo anatufahamisha kwamba ufalme wa Mungu ni ufalme wa uhalisia—sheria za milele za muundo (design laws) zinazoongoza shughuli za asili—na kwa hiyo ufalme wa Mungu haufanyi kazi kwa kanuni zilizobuniwa zinazohitaji adhabu za nje kama viumbe hufanya.

Paulo anaendelea kusema kwamba watu ambao hawajaletewa Neno la Mungu lililoandikwa, lakini wanaelewa uhalisia wa ufalme wa Mungu wa ukweli, upendo, na uhuru unaofunuliwa kupitia sheria za ubunifu wa uumbaji zilizojengwa katika asili, na hivyo kuchagua kumwamini, hupokea moyo mpya na roho iliyo sahihi, na sheria ya Mungu huandikwa mioyoni mwao. Wanakuwa washiriki wa agano jipya la wokovu (Waebrania 8:10).

“Wote watendao dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, na wote watendao dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria [Torati]. Kwa maana si wale wanaosikia sheria ndio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaotii sheria atakaotangazwa kuwa wenye haki. (Hakika, watu wa mataifa, wasio na sheria, wanafanya kwa asili mambo yanayotakiwa na sheria, wao wenyewe ni sheria kwao, ingawa hawana sheria, kwa kuwa wanaonyesha kwamba matakwa ya sheria yameandikwa mioyoni mwao, dhamiri zao zikiwa mashahidi, na mawazo yao mara nyingine yakiwashitaki, mara nyingine hata yakiwatetea.)” (Warumi 2:12–15, NIV84, msisitizo wangu).

Paulo anaeleza uhalisia kwamba sheria za ubunifu wa Mungu zimejengwa ndani ya jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Hata kama hakuna mtu anayekufundisha shuleni, wala husomi katika kitabu, lakini unazitambua katika asili na kuishi kwa upatanifu nazo kwa sababu unazithamini na kuzichagua, basi umechagua kumwamini Muumba, na Roho Mtakatifu hufanya kazi moyoni mwako kuandika sheria yake ndani yako. Kupitia ushindi wa Kristo, Roho Mtakatifu huleta maisha ya Kristo—ya ukweli, upendo, na uhuru—sheria za ubunifu wa Mungu—na kuzizalisha katika akili na moyo wako; huo ndio uzoefu wa agano jipya. Hata kama mtu bado hajasikia jina la Yesu, bado anaokolewa naye kwa sababu Yeye ni Muumba na Mtegemezaji wa asili. Uponyaji huu, mabadiliko, urejesho wa moyo na akili hauwezi kufanywa kwa njia za kisheria za nje.

Kuwa makini na kile Paulo anaandika baadaye:

Basi wewe unayejiita Myahudi; unayelitegemea torati na kujisifu kwa uhusiano wako na Mungu; unayejua mapenzi yake na kuidhinisha yaliyo bora kwa kuwa umefundishwa na torati; unayejiaminisha kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, nuru kwa walio gizani, mwalimu wa wapumbavu, mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una umbo la maarifa na ukweli katika torati—wewe basi unayefundisha wengine, hujifundishi? Wewe uhubiriye usiibe, waiba? Wewe usemaye watu wasizini, wazini? Wewe uchukiaye sanamu, waibia mahekalu? Wewe ujisifuye kwa torati, wamheshimu Mungu kwa kuivunja torati? Kama ilivyoandikwa: “Jina la Mungu linakufuriwa kati ya Mataifa kwa sababu yenu.” (Warumi 2:17–24 NIV).

Paulo anakabiliana na njia ya utii inayotegemea sheria zilizowekwa kwa nguvu, dini ya kisheria, na kutunza kanuni. Hii ni sawa na kuwaambia madaktari:

“Enyi mnaojiita viongozi wa huduma ya afya, mnaotegemea maarifa ya vitabu vyenu vya udaktari na kujisifu kwamba mna elimu zaidi; mkijiona kuwa waongoza wagonjwa kwa sababu mna vitabu—mbona hamjifundishi kuishi kwa afya? Kwa nini hamwachi kuvuta sigara? Kwa nini hamwachi kunywa pombe? Kwa nini hampati saa nane za usingizi kila usiku? Ninyi mnaochukia magonjwa kwa wengine na kujisifu kwa utaalamu wenu, kwa nini mnamdharau Mungu kwa kuvunja sheria zake za afya kwa jinsi mnavyoishi? Kama ilivyoandikwa, Mungu anawakilishwa vibaya kwa sababu yenu.”

Baada ya Paulo kuwaonya kwa kuwa na mtazamo wa kisheria wa dini huku wakiishi kinyume na sheria za ubunifu was Mungu katka uumbaji, anaandika:

Kwa kweli, Mataifa wasiotahiriwa wanaoitunza sheria ya Mungu watawahukumu ninyi Wayahudi mliotahiriwa na mnao torati lakini hamtiii (Warumi 2:27 NLT).

Paulo anasema kwamba wale ambao hawajawahi kwenda shule ya udaktari lakini wanaishi kwa upatanifu na sheria za afya za Mungu watawahukumu madaktari walio na vitabu lakini wanavunja sheria za afya.

Kisha anaeleza kwamba tohara si ya kisheria, ya tabia, au ya nje, bali ni tohara ya moyo kwa Roho—uhalisia—kukata roho ya hofu na ubinafsi na kuanzisha utambulisho wetu juu ya Roho Mtakatifu wa Mungu – maisha ya Kristo, roho ya upendo na uaminifu, inayoturejesha katika upatanifu na sheria za muundo za Mungu kwa maisha.

Paulo anaendelea kusisitiza kwamba sheria zilizowekwa kwa nguvu, dini ya kisheria, na utendaji wa nje havina nguvu ya kuokoa. Wokovu ni uhalisia wa Yesu kurejesha sheria yake hai ya upendo ndani ya ubinadamu. Katika Warumi 3 tunasoma:

Lakini sasa Mungu ameifunua hali ya afya ya ndani—tabia iliyo sawa na kamilifu kwa kila njia—ambayo haikutokana na maandiko ya kisheria, bali ndiyo ile ambayo Maandiko na Amri Kumi zilikuwa zikielekeza akili zenu. Hali hii kamilifu hutoka kwa Kristo na huumbwa ndani yetu na Mungu tunapomwamini. Uaminifu wetu kwake huanzishwa kwa ushahidi uliotolewa kupitia Yesu Kristo wa uaminifu wake wa juu kabisa. Hakuna tofauti kati ya makabila, kwa maana wanadamu wote wameambukizwa ugonjwa ule ule—wa kutoamini, hofu, na ubinafsi—na wamepotoshwa katika tabia na kukosa sana kiwango cha utukufu wa Mungu kwa ubinadamu. Hata hivyo, wote walio tayari huponywa bure kwa Dawa ya neema ya Mungu iliyotolewa na Yesu Kristo. Mungu alimtoa Yesu kama njia na chombo cha urejesho. Sasa, kupitia uaminifu uliowekwa kwa ushahidi wa tabia ya Mungu uliofunuliwa Kristo alipokufa, tunaweza kushiriki Dawa hiyo iliyopatikana kwa njia ya Kristo. Mungu alifanya hivi kuonyesha kwamba yeye ni wa haki na mwema—kwa maana kwa uvumilivu wake alisimamisha kwa muda matokeo ya mwisho ya kutokuwa katika upatanifu na muundo wake wa maisha—ingawa ameshtakiwa kwa uongo kuwa si wa haki. Alifanya hivi kuonyesha kwa wakati huu jinsi alivyo wa haki na mwema, ili aonekane kuwa wa haki anapowaponya wanaomwamini Yesu. (Warumi 3:21–26 Remedy).

Paulo anaendelea na hoja hii katika Warumi, lakini tukiruka hadi sura ya 14, anahitimisha tatizo kuu la dhambi:

Kila kisichotokana na imani ni dhambi (Warumi 14:23 NIV).

Hili ndilo tatizo, swali husika, kiini cha wokovu. Kwa msingi wake, dhambi ni kutomwamini Mungu. Adamu na Hawa walimkosa Mungu kwa kutoamini, na kutoamini kwao kulibadilisha roho yao kutoka upendo na uaminifu kwenda hofu na ubinafsi. Hofu na ubinafsi husababisha watu kutenda ili kujilinda na kujikuza—ambayo ni kinyume cha upendo.

Kwa sababu ya dhambi ya Adamu, tunazaliwa na roho ya hofu na ubinafsi, na wokovu unahitaji tuzaliwe upya kwa Roho/uzima wa Yesu—roho ya upendo na uaminifu. Hili haliwezi kutimizwa kwa sheria zilizowekwa kwa nguvu na utekelezaji wake. Kwa kweli, sheria zilizowekwa kwa nguvu huongeza hofu na kupunguza uaminifu na upendo. Uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi kama sheria za kibinadamu husababisha dini za kisheria kama ile ya Wayahudi waliomsulubisha Kristo; lakini wokovu unahitaji kuzaliwa upya.

Utii anaoutamani Mungu si kufanana kwa tabia ya kutunza kanuni, bali ni utii wa marafiki wanaopenda, mioyo yao imebadilishwa kutoka kutoamini, hofu, na ubinafsi kwenda ukweli, upendo, na uaminifu. Hili hutimizwa tu kwa njia za Mungu za ukweli na upendo; ndiyo maana Biblia inasema:

“Si kwa nguvu wala kwa uwezo, bali kwa Roho yangu,” asema BWANA wa majeshi (Zekaria 4:6 NIV).

Mungu hawezi kushinda, wala kurejesha upendo na uaminifu mioyoni na akilini kwa kutumia nguvu na uwezo; hufanya hivyo kwa Roho wake wa ukweli na upendo.

Utii wa kweli ni utii unaochipuka kutoka kwa upendo na uaminifu kwa Mungu, unaotoka katika moyo uliozaliwa upya na unaochochewa na Roho wa Kristo.

Nakuhimiza ukatae uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi kama sheria za kibinadamu, na urejee kumwabudu Mungu kama Muumba, ukitambua kwamba sheria zote za Mungu ni sheria za ubunifu wa uumbaji zilizojengwa ndani ya jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Kisha, kama bado hujafanya hivyo, fungua moyo wako kwake na uzaliwe upya katika uzima tele ambamo utii wa kweli unawezekana—utiifu wa upendo na uaminifu!

 

 

Donate online, securely via PayPal using your credit or debit card (no PayPal account needed, unless you want to set up a monthly, recurring payment).


cancel recurring payment

 

Want to use zelle instead?
See how on our
Support and Donations page.

Upcoming Events

calendar

Testimonial Post Slider

Testimony 28

I have been following your Bible study class for about a year now. I must say I am impressed with how your ministry has grown. I took it upon myself to listen to all your lesson podcasts from the past and they have both enriched me physically, mentally, emotionally and spiritually. I have learnt a lot from this class. I have also noticed how the class has grown in spiritual strength. One of the things that benefited me is that now I am not afraid of God. I use to be, but now it has melted away. The second thing is that you helped me to have a real life relationship with God. Now He is my friend that was always there and I love having him with me all the time. Thirdly, because of this class, it inspired me to take over and lead a class. I have called it “Let Us Reason Together,” adapting your inquisitive style and creating a class of free thinkers.

T. Banda, Malawi, Africa

 

Testimony 55

I was born [into the church], then I left it for many years. 10 years ago, I came back, but I could not take the hypocrisy and the lack of answers to the missing pieces. I struggled, but I did not abandon my commitment to know the truth. God is leading me to the simple understanding of his relevance and I am relearning what the church taught me as a youth… that he loves me, that he has led me to a knowledge of him such as I have never known. He is using Dr. Jennings to connect the dots that are now so apparent and hiding in plain sight!

Dean P., Arlington, TX, USA

 

Testimony 71

When I was 9 years old, I remember setting at our devotional table with a hunger and thirst for God that wanted more, deeper, BETTER. I can remember literally crying and pounding on the table, “I know these teachers didn’t mean to give us error. They taught what THEY had been TAUGHT, but didn’t ANYBODY READ THE BOOK?!?!?” It mattered to me then. It mattered to me as a teenager. It matters now as I teach bible classes. It didn’t have to be so hard as I watched so many give up and lay God’s great plan and gift of salvation aside as being “impossible.” Then, a friend sent me a link to Come And Reason’s website. I grew excited. YES! FINALLY! Then another friend told me to stay away, saying her son had just broken up with a girl because she was involved with Come And Reason and that “Tim Jennings preaches a false gospel.” But, AFTER many years of developing an authentic and, dare I say FUN relationship with Jesus, through the Holy Spirit I see this message has been around a LONG time, since the apostle Paul, Ellen White, Graham Maxwell, Ray Foucher, and yourself (though I admit, you’ve made me back up, rewind and replay the clips, and get out my well-worn Bible on a few things.) I’m so thankful I have found LIGHT during these DARK days. I am not alone.

Vicki DiNitto

Testimony 20

I just wanted to personally thank you for your teachings and insight into scripture. I came across your website via my cousin who suggested I look into “Healing the Mind” information. My youngest daughter has been struggling over the last couple of years and it all came to a head this spring. When I started listening to the “Healing the Mind” lectures my own life began to be transformed. I began sharing with all my daughters the concepts you laid out so clearly. I ordered your book and soaked it up. I just want to say “Thank You!” My walk with the Lord has been refreshed and renewed. Your obedience to the Lord is a blessing to so many.

R. K., Anderson, SC, USA

 

Testimony 5

We listen to your bible studies lessons in our class in Montana. You actually were the main reason I decided to get a laptop, so I can go to your site and listen, read, learn, and print the class notes. I am so grateful to learn the correct view of God and his character. Now, to just have others have an interest in knowing, so I can share it with them. Good thoughts your way.

R. N., MT, USA

 

Testimony 9

I really enjoy with you the view of a gracious God. Thank you for sharing the work you are allowing the Lord to do in you.

L., Queensland, Australia

 

Testimony 47

I can’t even begin to thank you and your ministry enough for introducing me to the Truth about a loving and merciful God! I have my daughter and her in-laws to thank for sharing with me “The God-Shaped Brain” as well as your website. I listen to the Bible study class lessons on my daily walk. May God continue to bless your thirst-quenching ministry!

Liz H., Port Angeles, WA, USA

 

 

Testimony 17

The blessings of clarity and understanding you and your class inspire me to take from the word of God have impressed upon me so greatly the true, loving character of our Creator. I have found amazing freedom and joy through building a stronger, more intentional relationship with Him. What is new is that this is now a relationship built on love, reverence and respect rather than fear and obligation, and as such my eyes have been slammed OPEN as I am continually impressed by the manifestations of God’s true character in His provisions for fallen man.

T.E.H., Salt Lake City, UT, USA

 

Testimony 1

Thank you! I love listening to the Come And Reason Ministries Bible study classes and am using some of your notes to get the lessons together that I will be teaching. You always have such good quotes and Bible texts and pull things together to make good sense.

T. C., IN, USA

 

Testimony 39

[This ministry is the] biggest blessing I have ever received! Your DVDs and lessons could not have come at a better time in my life. I have experienced in the past year many difficulties that, if it wasn’t for this wonderful view of God that I have discovered through this ministry, I would not have been able to respond in love and forgiveness. My heart is being transformed everyday by the Calvary-looking God you teach. Hallelujah!! I have tears in my eyes as I write, because my life has taken a complete turn from where I was heading.

I am from Central America. Most of my family is scattered in different parts of the world and all have the same view of God that I had growing up; a distant, exacting, and ready-to-punish-us-with-tragedy type of God. So, I have been translating lessons for my family and, to my surprise, they have also been sharing them with others! I can already see the difference. My brother has often said, “Thank you for sharing, I have never heard it this way!” My other family members are taking an amazing turn from a message of “repent or burn” towards a loving God, pleading to us that we won’t reject him because he loves us eternally.

Bless you for all you do.

Sofia S., Ashfield, MA, USA

 

Testimony 10

I personally download and listen to each of Come And Reason Ministries Bible study class lessons and PDF study notes to use when teaching my class. Really appreciate the class especially when Dr. Jennings is teaching. Thank God there are persons like him doing His work and traveling to share His beliefs.

B. L.M., North Plains, OR, USA

 

Testimony 44

We were given a gift of the DVD set, “God and Your Brain,” and we just finished watching it. The truths in this are so powerful and truly an answer to a prayer. We’re seeing hope where once we thought God wasn’t answering our prayers to be free of certain mindsets. He answered with these DVDs and we are hungry for more. Thank you!

Daniel T., Easley, SC, USA

 

Testimony 75

Thank you so much for everything you do! Because of all these truths, I’m excited to be with Jesus! I always pray everyday, “COME TODAY, JESUS.” Before finding C&R, I was always praying for delays, “NOT TODAY OH GOD. I AM NOT READY.” I just need to share more, talk more bout this truth, so everybody will be excited for Jesus.

J C Shin

Testimony 57

You have helped make sense of thirty two years of confusion. The material you freely provide reorganized so much of my life into such a beautiful pattern that has always been hinted at from within, but misguided with my training and what I was experiencing externally. My filipno parents, who were converted from Catholicism to SDA, were sincere and did their best to raise me the right way and I have deep respect for them. However, being immigrants and not understanding the language made for a difficult transition as I was growing up, which also applied to my spiritual growth as I learned the patterns of religion. I have been listening to as many bible study classes and reading blog posts as my time in a work truck will allow, searching for the practical applications of where spirituality and reality meet, and I thank you for helping me find that. You have helped me reach a point in which I can truly say that I love God, that I believe He loves me, and, like David, I delight in His law. God bless.

Emmanuel V., Calgary, AB Canada

Testimony 58

I have been watching your videos in The Power of Love seminar and I must say these have liberated me and have improved my relationship with the Lord. I am no longer terrified of him as I was before following your teachings.

Thando N., South Africa