Call Us: 423 661-4734 | Email: requests@comeandreason.com      
JE, NI UTII WA IMANI AU WA SHERIA?

JE, NI UTII WA IMANI AU WA SHERIA?

Wana wa Israeli walipokaribia mwisho wa miaka yao 40 ya kutangatanga jangwani na walipokuwa karibu kuingia Kanaani, Yoshua aliyekuwa akiwaongoza alipokea ujumbe ufuatao kutoka kwa Mungu:

Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda kulingana na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kulia, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako. (Yoshua 1:7).

Unaelewaje maagizo haya? Unaposikia mwito wa kutii sheria ya Mungu, nini huja akilini mwako? Je, unafikiria sheria ya Mungu kama sheria za kibinadamu — kanuni zinazowekwa ambazo Mungu huzisimamia na kutekeleza kwa adhabu? Au unafikiria sheria ambazo Muumba aliweka katika utendaji wa uhalisia — sheria za fizikia, mvuto (gravity) , afya, na sheria za maadili?

Je, unasikia mwito wa Mungu wa utii kama vile mwito wa daktari wa kuishi kwa afya (katika mwafaka na sheria za afya), au unasikia mwito wa Mungu wa utii kama onyo la askari polisi la kutokukimbiza gari kwa mwendo kasi?

Ni ukweli wa kusikitisha wa historia kwamba sehemu kubwa ya Ukristo imekubali uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi sawa tu na sheria za wanadamu—kanuni zilizobuniwa na kutekelezwa kwa adhabu. Lakini hebu tuchunguze utii unaotokana na sheria, kanuni, vitisho vya adhabu, na utekelezaji wa sheria—ukilinganisha na utii unaotokana na upendo, uaminifu, ambao pia hujulikana kama imani. Kisha tuchunguze jinsi upendo na uaminifu vinavyopandwa katika mioyo na akili na kupelekea utii.

 

UTII WA SHERIA

Fikiria umesimama chini ya msalaba wakati Yesu anasulubiwa. Unazungumza na Kayafa na viongozi wengine wa dini ya Kiyahudi wanaomdhihaki, kumtesa, na kumsulubisha Kristo. Unadhani wangetoa majibu gani kwa maswali yafuatayo?

  • Je, ni muhimu kuwa na utii wa agano kwa Mungu? “Kabisa!” naweza kuwasikia wakisema, “Tunaishi kwa ili kutii agano—sisi sote tumetahiriwa ipasavyo kama agano linavyoagiza.”
  • Je, ni muhimu kuitii sheria ya Mungu? “Bila shaka. Na kama hawa wahalifu hawatakufa upesi, tutamwomba Pilato aharakishe vifo vyao ili tuweze kuitunza Sabato kulingana na sheria.”
  • Je, ni muhimu kuitii sheria ambayo Musa mtumishi wa Mungu alitupa? “Bila shaka! Maisha yetu yote tunaishi tukilenga kutii sheria hiyo.”

Na kama tungewauliza, “Kwa nini mnamsulubisha huyu mtu?” naweza kuwasikia wakijibu:

“Naam, umeshatueleza wewe mwenyewe—lazima tuwe watiifu kwa agano, lazima tutii sheria ya Mungu, lazima tutii sheria ambazo Mungu alitupatia kupitia Musa—na huyu mtu anazivunja mara kwa mara. Musa alituagiza tumpige kwa mawe mzinzi, lakini huyu mtu aliwasamehe. Musa alitupa ruhusa ya kuwataliki wake zetu, lakini huyu mtu alisema tusifanye hivyo. Musa alitufundisha tusifanye kazi siku ya Sabato, lakini huyu mtu aliwaponya wagonjwa siku ya Sabato na wanafunzi wake walivuna punje siku ya Sabato. Musa alitufundisha kuosha kwa namna fulani kabla ya kula, lakini huyu mtu hakuwaelekeza wanafunzi wake wafanye hivyo. Musa alitufundisha kwamba sheria lazima zitekelezwe na kwamba uovu lazima uondolewe katika jamii, na ndicho tunachofanya kwa sababu sisi ni watoto wa Abrahamu na wa Mungu, na tumejitoa kwa uaminifu na utii wa agano.”

Utii wa sheria na utekelezaji wa sheria hauna uwezo wa kubadili mioyo na akili, wala kusimika upendo, uaminifu, urafiki, uaminifu wa kudumu, na kujitoa. Utii wa uongozi wa Kiyahudi uliomsulubisha Kristo ulikuwa aina iliyowafanya wawe maadui wa Mungu huku wakidai kuwa watoto wake na kufanya kazi yake.

Mtume Paulo anashughulikia mwelekeo huu wote wa kisheria usio sahihi kuhusu utii katika kitabu cha Warumi, na analinganisha utii unaotokana na sheria na utii unaotokana na imani au uaminifu. Anaanza kitabu cha Warumi kwa kusema:

Kupitia yeye na kwa ajili ya jina lake, tumepokea neema na utume ili kuwaita watu kutoka mataifa yote katika utii unaotokana na imani. (Warumi 1:5).

Imani au uaminifu si kitu kinachoweza kuamriwa, kutungwa kwa sheria, kuagizwa, au kupatikana kwa njia ya sheria na utekelezaji wake. Uaminifu hujengwa juu ya uaminifu halisi wa maisha, unaohitaji ushahidi, ambao lazima ueleweke na kuishiwa. Uaminifu hauwezi kuanzishwa kwa tangazo, madai, amri, maagizo, kanuni, na masharti, na utadhoofishwa na vitisho na adhabu. Jaribu kupata uaminifu wa mtu kwa kumtishia kumdhuru au kumwadhibu ikiwa hatakuamini—haiwezekani kabisa! Sheria zilizolazimishwa na utekelezaji wake haziwezi kuvutia mioyo na akili, na hatimaye, zitawageuza wale wanaotumia mbinu hizo kama njia ya kutafuta haki kuwa waasi.

Paulo, akielewa hili, baada ya kutufundisha kwamba anawaita watu kwenye utii unaotokana na imani, anatueleza msingi wa imani hiyo. Katika Warumi 1:20 anaandika:

Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, sifa zisizoonekana za Mungu—uwezo wake wa milele na asili yake ya uungu—zimeonekana wazi, zikieleweka kutokana na mambo yaliyoumbwa, hivyo watu hawana udhuru (NIV msisitizo wangu).

Imani yetu kwa Mungu haijengwi juu ya madai, maneno, au amri, bali juu ya uhalisia, ushahidi, na ukweli. Mungu ni Muumba, na sheria zake ndizo sheria zinazoongoza jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Paulo anatufahamisha kwamba ufalme wa Mungu ni ufalme wa uhalisia—sheria za milele za muundo (design laws) zinazoongoza shughuli za asili—na kwa hiyo ufalme wa Mungu haufanyi kazi kwa kanuni zilizobuniwa zinazohitaji adhabu za nje kama viumbe hufanya.

Paulo anaendelea kusema kwamba watu ambao hawajaletewa Neno la Mungu lililoandikwa, lakini wanaelewa uhalisia wa ufalme wa Mungu wa ukweli, upendo, na uhuru unaofunuliwa kupitia sheria za ubunifu wa uumbaji zilizojengwa katika asili, na hivyo kuchagua kumwamini, hupokea moyo mpya na roho iliyo sahihi, na sheria ya Mungu huandikwa mioyoni mwao. Wanakuwa washiriki wa agano jipya la wokovu (Waebrania 8:10).

“Wote watendao dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, na wote watendao dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria [Torati]. Kwa maana si wale wanaosikia sheria ndio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaotii sheria atakaotangazwa kuwa wenye haki. (Hakika, watu wa mataifa, wasio na sheria, wanafanya kwa asili mambo yanayotakiwa na sheria, wao wenyewe ni sheria kwao, ingawa hawana sheria, kwa kuwa wanaonyesha kwamba matakwa ya sheria yameandikwa mioyoni mwao, dhamiri zao zikiwa mashahidi, na mawazo yao mara nyingine yakiwashitaki, mara nyingine hata yakiwatetea.)” (Warumi 2:12–15, NIV84, msisitizo wangu).

Paulo anaeleza uhalisia kwamba sheria za ubunifu wa Mungu zimejengwa ndani ya jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Hata kama hakuna mtu anayekufundisha shuleni, wala husomi katika kitabu, lakini unazitambua katika asili na kuishi kwa upatanifu nazo kwa sababu unazithamini na kuzichagua, basi umechagua kumwamini Muumba, na Roho Mtakatifu hufanya kazi moyoni mwako kuandika sheria yake ndani yako. Kupitia ushindi wa Kristo, Roho Mtakatifu huleta maisha ya Kristo—ya ukweli, upendo, na uhuru—sheria za ubunifu wa Mungu—na kuzizalisha katika akili na moyo wako; huo ndio uzoefu wa agano jipya. Hata kama mtu bado hajasikia jina la Yesu, bado anaokolewa naye kwa sababu Yeye ni Muumba na Mtegemezaji wa asili. Uponyaji huu, mabadiliko, urejesho wa moyo na akili hauwezi kufanywa kwa njia za kisheria za nje.

Kuwa makini na kile Paulo anaandika baadaye:

Basi wewe unayejiita Myahudi; unayelitegemea torati na kujisifu kwa uhusiano wako na Mungu; unayejua mapenzi yake na kuidhinisha yaliyo bora kwa kuwa umefundishwa na torati; unayejiaminisha kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, nuru kwa walio gizani, mwalimu wa wapumbavu, mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una umbo la maarifa na ukweli katika torati—wewe basi unayefundisha wengine, hujifundishi? Wewe uhubiriye usiibe, waiba? Wewe usemaye watu wasizini, wazini? Wewe uchukiaye sanamu, waibia mahekalu? Wewe ujisifuye kwa torati, wamheshimu Mungu kwa kuivunja torati? Kama ilivyoandikwa: “Jina la Mungu linakufuriwa kati ya Mataifa kwa sababu yenu.” (Warumi 2:17–24 NIV).

Paulo anakabiliana na njia ya utii inayotegemea sheria zilizowekwa kwa nguvu, dini ya kisheria, na kutunza kanuni. Hii ni sawa na kuwaambia madaktari:

“Enyi mnaojiita viongozi wa huduma ya afya, mnaotegemea maarifa ya vitabu vyenu vya udaktari na kujisifu kwamba mna elimu zaidi; mkijiona kuwa waongoza wagonjwa kwa sababu mna vitabu—mbona hamjifundishi kuishi kwa afya? Kwa nini hamwachi kuvuta sigara? Kwa nini hamwachi kunywa pombe? Kwa nini hampati saa nane za usingizi kila usiku? Ninyi mnaochukia magonjwa kwa wengine na kujisifu kwa utaalamu wenu, kwa nini mnamdharau Mungu kwa kuvunja sheria zake za afya kwa jinsi mnavyoishi? Kama ilivyoandikwa, Mungu anawakilishwa vibaya kwa sababu yenu.”

Baada ya Paulo kuwaonya kwa kuwa na mtazamo wa kisheria wa dini huku wakiishi kinyume na sheria za ubunifu was Mungu katka uumbaji, anaandika:

Kwa kweli, Mataifa wasiotahiriwa wanaoitunza sheria ya Mungu watawahukumu ninyi Wayahudi mliotahiriwa na mnao torati lakini hamtiii (Warumi 2:27 NLT).

Paulo anasema kwamba wale ambao hawajawahi kwenda shule ya udaktari lakini wanaishi kwa upatanifu na sheria za afya za Mungu watawahukumu madaktari walio na vitabu lakini wanavunja sheria za afya.

Kisha anaeleza kwamba tohara si ya kisheria, ya tabia, au ya nje, bali ni tohara ya moyo kwa Roho—uhalisia—kukata roho ya hofu na ubinafsi na kuanzisha utambulisho wetu juu ya Roho Mtakatifu wa Mungu – maisha ya Kristo, roho ya upendo na uaminifu, inayoturejesha katika upatanifu na sheria za muundo za Mungu kwa maisha.

Paulo anaendelea kusisitiza kwamba sheria zilizowekwa kwa nguvu, dini ya kisheria, na utendaji wa nje havina nguvu ya kuokoa. Wokovu ni uhalisia wa Yesu kurejesha sheria yake hai ya upendo ndani ya ubinadamu. Katika Warumi 3 tunasoma:

Lakini sasa Mungu ameifunua hali ya afya ya ndani—tabia iliyo sawa na kamilifu kwa kila njia—ambayo haikutokana na maandiko ya kisheria, bali ndiyo ile ambayo Maandiko na Amri Kumi zilikuwa zikielekeza akili zenu. Hali hii kamilifu hutoka kwa Kristo na huumbwa ndani yetu na Mungu tunapomwamini. Uaminifu wetu kwake huanzishwa kwa ushahidi uliotolewa kupitia Yesu Kristo wa uaminifu wake wa juu kabisa. Hakuna tofauti kati ya makabila, kwa maana wanadamu wote wameambukizwa ugonjwa ule ule—wa kutoamini, hofu, na ubinafsi—na wamepotoshwa katika tabia na kukosa sana kiwango cha utukufu wa Mungu kwa ubinadamu. Hata hivyo, wote walio tayari huponywa bure kwa Dawa ya neema ya Mungu iliyotolewa na Yesu Kristo. Mungu alimtoa Yesu kama njia na chombo cha urejesho. Sasa, kupitia uaminifu uliowekwa kwa ushahidi wa tabia ya Mungu uliofunuliwa Kristo alipokufa, tunaweza kushiriki Dawa hiyo iliyopatikana kwa njia ya Kristo. Mungu alifanya hivi kuonyesha kwamba yeye ni wa haki na mwema—kwa maana kwa uvumilivu wake alisimamisha kwa muda matokeo ya mwisho ya kutokuwa katika upatanifu na muundo wake wa maisha—ingawa ameshtakiwa kwa uongo kuwa si wa haki. Alifanya hivi kuonyesha kwa wakati huu jinsi alivyo wa haki na mwema, ili aonekane kuwa wa haki anapowaponya wanaomwamini Yesu. (Warumi 3:21–26 Remedy).

Paulo anaendelea na hoja hii katika Warumi, lakini tukiruka hadi sura ya 14, anahitimisha tatizo kuu la dhambi:

Kila kisichotokana na imani ni dhambi (Warumi 14:23 NIV).

Hili ndilo tatizo, swali husika, kiini cha wokovu. Kwa msingi wake, dhambi ni kutomwamini Mungu. Adamu na Hawa walimkosa Mungu kwa kutoamini, na kutoamini kwao kulibadilisha roho yao kutoka upendo na uaminifu kwenda hofu na ubinafsi. Hofu na ubinafsi husababisha watu kutenda ili kujilinda na kujikuza—ambayo ni kinyume cha upendo.

Kwa sababu ya dhambi ya Adamu, tunazaliwa na roho ya hofu na ubinafsi, na wokovu unahitaji tuzaliwe upya kwa Roho/uzima wa Yesu—roho ya upendo na uaminifu. Hili haliwezi kutimizwa kwa sheria zilizowekwa kwa nguvu na utekelezaji wake. Kwa kweli, sheria zilizowekwa kwa nguvu huongeza hofu na kupunguza uaminifu na upendo. Uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi kama sheria za kibinadamu husababisha dini za kisheria kama ile ya Wayahudi waliomsulubisha Kristo; lakini wokovu unahitaji kuzaliwa upya.

Utii anaoutamani Mungu si kufanana kwa tabia ya kutunza kanuni, bali ni utii wa marafiki wanaopenda, mioyo yao imebadilishwa kutoka kutoamini, hofu, na ubinafsi kwenda ukweli, upendo, na uaminifu. Hili hutimizwa tu kwa njia za Mungu za ukweli na upendo; ndiyo maana Biblia inasema:

“Si kwa nguvu wala kwa uwezo, bali kwa Roho yangu,” asema BWANA wa majeshi (Zekaria 4:6 NIV).

Mungu hawezi kushinda, wala kurejesha upendo na uaminifu mioyoni na akilini kwa kutumia nguvu na uwezo; hufanya hivyo kwa Roho wake wa ukweli na upendo.

Utii wa kweli ni utii unaochipuka kutoka kwa upendo na uaminifu kwa Mungu, unaotoka katika moyo uliozaliwa upya na unaochochewa na Roho wa Kristo.

Nakuhimiza ukatae uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi kama sheria za kibinadamu, na urejee kumwabudu Mungu kama Muumba, ukitambua kwamba sheria zote za Mungu ni sheria za ubunifu wa uumbaji zilizojengwa ndani ya jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Kisha, kama bado hujafanya hivyo, fungua moyo wako kwake na uzaliwe upya katika uzima tele ambamo utii wa kweli unawezekana—utiifu wa upendo na uaminifu!

 

 

Donate online, securely via PayPal using your credit or debit card (no PayPal account needed, unless you want to set up a monthly, recurring payment).


cancel recurring payment

 

Want to use zelle instead?
See how on our
Support and Donations page.

Upcoming Events

calendar

Testimonial Post Slider

Testimony 19

I truly believe that to know who God really is the first step to understand ourselves in a balanced and kind way, so the healing can take place. Your approach really makes sense – Thank you for your ministry!

A.M., Pittsburg, PA, USA

Testimony 37

Hearing Dr. Jennings’ presentations in person came at a pivotal moment in my spiritual journey that began about nine months ago, when the fault lines inherent in my belief system began to crack under questions that most reasonable people end up asking about God and His nature. These were questions I couldn’t find answers to, and they shook my faith. I was unable let it go any longer and be satisfied. My Christian experience became distant. I was afraid; the fear in me rose like thorns, pushing me away from Jesus. And then someone heard my questions and introduced me to this ministry, and my life has totally changed.

I can tell you that this new, “present truth” message is far grander and life-changing than when I shifted from being an agnostic and then a nominal Christian. It has radically altered my worldview, because it reveals a God that makes sense. It is a revolution. I believe that Dr. Jennings’ message is the final message that must go to the world. If any message could be called “righteousness by faith,” as abused as that term is by the right and the left, this is that message, because Jennings’ biblical message identifies a God who is different, whose character isn’t an impossible contradiction.

I walk this path now without fear. I see people differently, and the Holy Spirit burns in my heart. Many call Dr. Jennings’ message false and compromising, but it isn’t false, because I’ve seen the fruits within my mind and body. It is not compromising, because in this message is the only road to holiness that makes any sense. No longer do I behold a pagan god who is always angry and suspicious. Instead, I behold a God who is freeing and loving, always working for our good, and giving me every reason to love my enemy even to my own death, just as Jesus pleads with us. God is good.

Anthony L., CA, USA

 

Testimony 21

I am absolutly on fire with the message at Come and Reason! I can’t get enough! I’ve read your book, blog, and articles. I’ve listened to your Bible study podcasts, your radio show, and your series – all excellent! It wasn’t until the past couple of years that I have I like I’m becoming “healthy,” with more to share with others than just beasts and commandments! I used to be a Bible worker and preached when the pastors were gone until I had had enough. I didnt realize at the time what the problem was, but i know now… the message wasn’t properly focused. Now my flame is rekindled. All of your little examples are so perfect in explaining something “complicated” and making it easily understood! Now I’m trying to shape it into a life changing evangelistic series! Thank you!

M.T., USA

 

Testimony 67

I was introduced to Come And Reason by a friend of my mother-in-law, who gave me several CD’s of Dr. Jennings. The clarity of the message and recognition that God’s is a God of love was so clear, advancing beyond Dr. Maxwell’s message. However, grappled with Maxwell saying God used emergency measures for the fallen world. Now after several years of being a regular listener of the Come And Reasoning bible study class and attending Jennings’ meetings in Dallas/Fort Worth, TX, things are becoming clearer for me. Design law versus imposed law has added so much to my personal understanding of theology. This message has really impacted my work in counseling so many people miserable because they are searching for and trusting human governments to create order and peace or believing in a God who says love Me or I will kill you. I am grateful that I have an alternative view to offer my clients that makes sense. I teach a bible study class on a semi-regular basis and I value the materials that Come And Reason so freely offers to aid me in presenting this vital message. Thank you for continuing to provide advancement in our very limited understanding of a Infinite God that is rational and believable.

Dr. Roger D, Arlington, TX, USA

 

Testimony 43

Two years ago I stumbled upon your book, “Could It Be This Simple,” and then found “The God-Shaped Brain” videos on YouTube, your bible study class, and the ‘Come And Reason’ mobile app. I shared your book with a friend and after nine months of showing love, patience, and kindness this person has been changed by the love of God, too. The same love that healed me, I now express to other women in tangible ways, such as to a Baptist woman with high anxiety and childhood trauma. She was extremely happy and relieved when I shared about the so-called “judgment of God” and burning in hell. She had no desire to serve a God that was so harsh. I have repeated the phrase dozens of times to her. “What we believe has power over us, but we have power over what we believe…”

This message that you are sharing has changed my life. I will continue to serve other women and bring this message of God’s healing love to their lives by sharing your books, YouTube videos, and The Remedy Bible app. Keep up the good work. Don’t be discouraged. God is doing a mighty work in and through this ministry!

Jill L., Midwest, USA

 

Testimony 57

You have helped make sense of thirty two years of confusion. The material you freely provide reorganized so much of my life into such a beautiful pattern that has always been hinted at from within, but misguided with my training and what I was experiencing externally. My filipno parents, who were converted from Catholicism to SDA, were sincere and did their best to raise me the right way and I have deep respect for them. However, being immigrants and not understanding the language made for a difficult transition as I was growing up, which also applied to my spiritual growth as I learned the patterns of religion. I have been listening to as many bible study classes and reading blog posts as my time in a work truck will allow, searching for the practical applications of where spirituality and reality meet, and I thank you for helping me find that. You have helped me reach a point in which I can truly say that I love God, that I believe He loves me, and, like David, I delight in His law. God bless.

Emmanuel V., Calgary, AB Canada

Testimony 33

I was invited over a friend’s house to see the “God and Your Brain” seminar today. I became [a christian] 36 years ago at the age of 19, but have struggled with the concept of God taking His ‘pound of flesh’ out on His Son to be appeased. Wow. Your seminar has been an incredible revelation and breath of reason and fresh air! I have your book, “The God Shaped Brain,” and it is SO eye opening. Finally, after 36 years enlightenment has come! Praise the Good Lord! What can I say, but that the Real Gospel is truly “Good News!” Thank you for your efforts in giving the Gospel a clear sound!

Paul C.,  Springfield, MA, USA

 

Testimony 27

Your teachings about our heavenly Father have changed my life. Thank you sooooooo very very much! I know He’s doing some serious healing in my heart and life and I look forward to each new day to learn something new about Him and to just hear you speak about Him. Thank you, forever.

Nancy S.

 

Testimony 12

I have been really blessed reading your response to the various questions on your site.

K.C., OH, USA

 

Testimony 6

I got the book “Could It Be This Simple?” a few months ago and the reading was wonderful and I was fascinated. I lent the book to a friend at work. She is having a difficult time and the book is helping her to find Jesus and I found this very exciting. She has asked me questions and I can see her life changing.

H. S., Australia

 

Testimony 60

Just watched watched lesson 10 in the 1st quarter 2021 bible study classs on Isaiah. I want to thank you for your intellectual spirituality; it’s not an oxymoron! From the point of view of a teacher I also enjoy seeing how much personal pleasure you clearly take in not just tasting, but feasting on God’s word – it reminds me of Jeremiah not being able to hold it in! It makes me smile that your cup is so full and overflowing that you make it to Tuesday’s lesson (on a good day). It just goes to show the richness of God’s Word.

God bless the Come and Reason Team from our church here in Great Britain.

Andrew H., Great Britain

 

Testimony 15

I have been sharing Come And Reason Ministries Bible study lessons with several folk. You have such a beautiful view of the plan of salvation. If we had this message preached when I was young, my generation would still all be in church.

H. R., New Zealand

Testimony 34

I was introduced to Come and Reason Ministries by accident, via a passing comment made in a bible study class we were visiting. I checked this website out and my life was changed. The understanding of the truth of God’s character, and how we apply it, is so right. The tricky part is consistently applying which “lens” to look through. As I began to understand, I started sharing the basics of this understanding with a discussion group I was leading and, suddenly, a lot of things started to make sense that never used to. At the same time, I enjoyed an amazing opportunity. I was able to conduct a full bible study at WORK! What an amazing experience! It is such a joy to share the truth about God and to share how it all fits in the war between God and Satan. So many people benefit when we have a correct understanding about how God works and who He really is! Thank you for this transformational understanding. Keep up the good work! God Bless you!

Tony P., CA, USA

 

Testimony 41

I have been blessed by your ministry. I have experienced personally, and deeply resonate with, the God of love and the beautiful picture of God’s character that you present. I have seen your seminar series on YouTube, read ‘The Journal of the Watcher’ book, used your mobile app, and also listen/study the bible study lesson with you each week. I concur with many of the thoughts and perspectives that you share. I understand your conclusions on natural laws vs imposed law and the legal/penal substitution (incorrect diagnosis). This makes perfect sense to me.

Bless you for all you do.

Melissa L.

 

Testimony 70

I have been watching you for many years and have learned to love God with all my heart. I was raised by a loving Christian mother that had been lied to about who God really was, so our religious upbringing was hell fire and damnation. As soon as I was old enough and moved out, I not only left the church, I ran as fast as I could to get away from it. Sad to say, it wasn’t until the past couple of years that I learned and understand who my Father really is and how much He loves me. I understand God’s Design Laws (which make sense) and when I’m teaching my church Bible study class, I’m able to really put to use the things I’ve been learning and Holy Spirit is leading. Thank you for introducing me to my Father of true, pure love. Everyday with Him is new and exciting. One thing that breaks my heart is that I didn’t know Him sooner. God Bless you and your ministry!

Judy Phelps, Reno, NV, USA