Call Us: 423 661-4734 | Email: requests@comeandreason.com      
JE, NI UTII WA IMANI AU WA SHERIA?

JE, NI UTII WA IMANI AU WA SHERIA?

Wana wa Israeli walipokaribia mwisho wa miaka yao 40 ya kutangatanga jangwani na walipokuwa karibu kuingia Kanaani, Yoshua aliyekuwa akiwaongoza alipokea ujumbe ufuatao kutoka kwa Mungu:

Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda kulingana na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kulia, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako. (Yoshua 1:7).

Unaelewaje maagizo haya? Unaposikia mwito wa kutii sheria ya Mungu, nini huja akilini mwako? Je, unafikiria sheria ya Mungu kama sheria za kibinadamu — kanuni zinazowekwa ambazo Mungu huzisimamia na kutekeleza kwa adhabu? Au unafikiria sheria ambazo Muumba aliweka katika utendaji wa uhalisia — sheria za fizikia, mvuto (gravity) , afya, na sheria za maadili?

Je, unasikia mwito wa Mungu wa utii kama vile mwito wa daktari wa kuishi kwa afya (katika mwafaka na sheria za afya), au unasikia mwito wa Mungu wa utii kama onyo la askari polisi la kutokukimbiza gari kwa mwendo kasi?

Ni ukweli wa kusikitisha wa historia kwamba sehemu kubwa ya Ukristo imekubali uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi sawa tu na sheria za wanadamu—kanuni zilizobuniwa na kutekelezwa kwa adhabu. Lakini hebu tuchunguze utii unaotokana na sheria, kanuni, vitisho vya adhabu, na utekelezaji wa sheria—ukilinganisha na utii unaotokana na upendo, uaminifu, ambao pia hujulikana kama imani. Kisha tuchunguze jinsi upendo na uaminifu vinavyopandwa katika mioyo na akili na kupelekea utii.

 

UTII WA SHERIA

Fikiria umesimama chini ya msalaba wakati Yesu anasulubiwa. Unazungumza na Kayafa na viongozi wengine wa dini ya Kiyahudi wanaomdhihaki, kumtesa, na kumsulubisha Kristo. Unadhani wangetoa majibu gani kwa maswali yafuatayo?

  • Je, ni muhimu kuwa na utii wa agano kwa Mungu? “Kabisa!” naweza kuwasikia wakisema, “Tunaishi kwa ili kutii agano—sisi sote tumetahiriwa ipasavyo kama agano linavyoagiza.”
  • Je, ni muhimu kuitii sheria ya Mungu? “Bila shaka. Na kama hawa wahalifu hawatakufa upesi, tutamwomba Pilato aharakishe vifo vyao ili tuweze kuitunza Sabato kulingana na sheria.”
  • Je, ni muhimu kuitii sheria ambayo Musa mtumishi wa Mungu alitupa? “Bila shaka! Maisha yetu yote tunaishi tukilenga kutii sheria hiyo.”

Na kama tungewauliza, “Kwa nini mnamsulubisha huyu mtu?” naweza kuwasikia wakijibu:

“Naam, umeshatueleza wewe mwenyewe—lazima tuwe watiifu kwa agano, lazima tutii sheria ya Mungu, lazima tutii sheria ambazo Mungu alitupatia kupitia Musa—na huyu mtu anazivunja mara kwa mara. Musa alituagiza tumpige kwa mawe mzinzi, lakini huyu mtu aliwasamehe. Musa alitupa ruhusa ya kuwataliki wake zetu, lakini huyu mtu alisema tusifanye hivyo. Musa alitufundisha tusifanye kazi siku ya Sabato, lakini huyu mtu aliwaponya wagonjwa siku ya Sabato na wanafunzi wake walivuna punje siku ya Sabato. Musa alitufundisha kuosha kwa namna fulani kabla ya kula, lakini huyu mtu hakuwaelekeza wanafunzi wake wafanye hivyo. Musa alitufundisha kwamba sheria lazima zitekelezwe na kwamba uovu lazima uondolewe katika jamii, na ndicho tunachofanya kwa sababu sisi ni watoto wa Abrahamu na wa Mungu, na tumejitoa kwa uaminifu na utii wa agano.”

Utii wa sheria na utekelezaji wa sheria hauna uwezo wa kubadili mioyo na akili, wala kusimika upendo, uaminifu, urafiki, uaminifu wa kudumu, na kujitoa. Utii wa uongozi wa Kiyahudi uliomsulubisha Kristo ulikuwa aina iliyowafanya wawe maadui wa Mungu huku wakidai kuwa watoto wake na kufanya kazi yake.

Mtume Paulo anashughulikia mwelekeo huu wote wa kisheria usio sahihi kuhusu utii katika kitabu cha Warumi, na analinganisha utii unaotokana na sheria na utii unaotokana na imani au uaminifu. Anaanza kitabu cha Warumi kwa kusema:

Kupitia yeye na kwa ajili ya jina lake, tumepokea neema na utume ili kuwaita watu kutoka mataifa yote katika utii unaotokana na imani. (Warumi 1:5).

Imani au uaminifu si kitu kinachoweza kuamriwa, kutungwa kwa sheria, kuagizwa, au kupatikana kwa njia ya sheria na utekelezaji wake. Uaminifu hujengwa juu ya uaminifu halisi wa maisha, unaohitaji ushahidi, ambao lazima ueleweke na kuishiwa. Uaminifu hauwezi kuanzishwa kwa tangazo, madai, amri, maagizo, kanuni, na masharti, na utadhoofishwa na vitisho na adhabu. Jaribu kupata uaminifu wa mtu kwa kumtishia kumdhuru au kumwadhibu ikiwa hatakuamini—haiwezekani kabisa! Sheria zilizolazimishwa na utekelezaji wake haziwezi kuvutia mioyo na akili, na hatimaye, zitawageuza wale wanaotumia mbinu hizo kama njia ya kutafuta haki kuwa waasi.

Paulo, akielewa hili, baada ya kutufundisha kwamba anawaita watu kwenye utii unaotokana na imani, anatueleza msingi wa imani hiyo. Katika Warumi 1:20 anaandika:

Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, sifa zisizoonekana za Mungu—uwezo wake wa milele na asili yake ya uungu—zimeonekana wazi, zikieleweka kutokana na mambo yaliyoumbwa, hivyo watu hawana udhuru (NIV msisitizo wangu).

Imani yetu kwa Mungu haijengwi juu ya madai, maneno, au amri, bali juu ya uhalisia, ushahidi, na ukweli. Mungu ni Muumba, na sheria zake ndizo sheria zinazoongoza jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Paulo anatufahamisha kwamba ufalme wa Mungu ni ufalme wa uhalisia—sheria za milele za muundo (design laws) zinazoongoza shughuli za asili—na kwa hiyo ufalme wa Mungu haufanyi kazi kwa kanuni zilizobuniwa zinazohitaji adhabu za nje kama viumbe hufanya.

Paulo anaendelea kusema kwamba watu ambao hawajaletewa Neno la Mungu lililoandikwa, lakini wanaelewa uhalisia wa ufalme wa Mungu wa ukweli, upendo, na uhuru unaofunuliwa kupitia sheria za ubunifu wa uumbaji zilizojengwa katika asili, na hivyo kuchagua kumwamini, hupokea moyo mpya na roho iliyo sahihi, na sheria ya Mungu huandikwa mioyoni mwao. Wanakuwa washiriki wa agano jipya la wokovu (Waebrania 8:10).

“Wote watendao dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, na wote watendao dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria [Torati]. Kwa maana si wale wanaosikia sheria ndio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaotii sheria atakaotangazwa kuwa wenye haki. (Hakika, watu wa mataifa, wasio na sheria, wanafanya kwa asili mambo yanayotakiwa na sheria, wao wenyewe ni sheria kwao, ingawa hawana sheria, kwa kuwa wanaonyesha kwamba matakwa ya sheria yameandikwa mioyoni mwao, dhamiri zao zikiwa mashahidi, na mawazo yao mara nyingine yakiwashitaki, mara nyingine hata yakiwatetea.)” (Warumi 2:12–15, NIV84, msisitizo wangu).

Paulo anaeleza uhalisia kwamba sheria za ubunifu wa Mungu zimejengwa ndani ya jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Hata kama hakuna mtu anayekufundisha shuleni, wala husomi katika kitabu, lakini unazitambua katika asili na kuishi kwa upatanifu nazo kwa sababu unazithamini na kuzichagua, basi umechagua kumwamini Muumba, na Roho Mtakatifu hufanya kazi moyoni mwako kuandika sheria yake ndani yako. Kupitia ushindi wa Kristo, Roho Mtakatifu huleta maisha ya Kristo—ya ukweli, upendo, na uhuru—sheria za ubunifu wa Mungu—na kuzizalisha katika akili na moyo wako; huo ndio uzoefu wa agano jipya. Hata kama mtu bado hajasikia jina la Yesu, bado anaokolewa naye kwa sababu Yeye ni Muumba na Mtegemezaji wa asili. Uponyaji huu, mabadiliko, urejesho wa moyo na akili hauwezi kufanywa kwa njia za kisheria za nje.

Kuwa makini na kile Paulo anaandika baadaye:

Basi wewe unayejiita Myahudi; unayelitegemea torati na kujisifu kwa uhusiano wako na Mungu; unayejua mapenzi yake na kuidhinisha yaliyo bora kwa kuwa umefundishwa na torati; unayejiaminisha kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, nuru kwa walio gizani, mwalimu wa wapumbavu, mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una umbo la maarifa na ukweli katika torati—wewe basi unayefundisha wengine, hujifundishi? Wewe uhubiriye usiibe, waiba? Wewe usemaye watu wasizini, wazini? Wewe uchukiaye sanamu, waibia mahekalu? Wewe ujisifuye kwa torati, wamheshimu Mungu kwa kuivunja torati? Kama ilivyoandikwa: “Jina la Mungu linakufuriwa kati ya Mataifa kwa sababu yenu.” (Warumi 2:17–24 NIV).

Paulo anakabiliana na njia ya utii inayotegemea sheria zilizowekwa kwa nguvu, dini ya kisheria, na kutunza kanuni. Hii ni sawa na kuwaambia madaktari:

“Enyi mnaojiita viongozi wa huduma ya afya, mnaotegemea maarifa ya vitabu vyenu vya udaktari na kujisifu kwamba mna elimu zaidi; mkijiona kuwa waongoza wagonjwa kwa sababu mna vitabu—mbona hamjifundishi kuishi kwa afya? Kwa nini hamwachi kuvuta sigara? Kwa nini hamwachi kunywa pombe? Kwa nini hampati saa nane za usingizi kila usiku? Ninyi mnaochukia magonjwa kwa wengine na kujisifu kwa utaalamu wenu, kwa nini mnamdharau Mungu kwa kuvunja sheria zake za afya kwa jinsi mnavyoishi? Kama ilivyoandikwa, Mungu anawakilishwa vibaya kwa sababu yenu.”

Baada ya Paulo kuwaonya kwa kuwa na mtazamo wa kisheria wa dini huku wakiishi kinyume na sheria za ubunifu was Mungu katka uumbaji, anaandika:

Kwa kweli, Mataifa wasiotahiriwa wanaoitunza sheria ya Mungu watawahukumu ninyi Wayahudi mliotahiriwa na mnao torati lakini hamtiii (Warumi 2:27 NLT).

Paulo anasema kwamba wale ambao hawajawahi kwenda shule ya udaktari lakini wanaishi kwa upatanifu na sheria za afya za Mungu watawahukumu madaktari walio na vitabu lakini wanavunja sheria za afya.

Kisha anaeleza kwamba tohara si ya kisheria, ya tabia, au ya nje, bali ni tohara ya moyo kwa Roho—uhalisia—kukata roho ya hofu na ubinafsi na kuanzisha utambulisho wetu juu ya Roho Mtakatifu wa Mungu – maisha ya Kristo, roho ya upendo na uaminifu, inayoturejesha katika upatanifu na sheria za muundo za Mungu kwa maisha.

Paulo anaendelea kusisitiza kwamba sheria zilizowekwa kwa nguvu, dini ya kisheria, na utendaji wa nje havina nguvu ya kuokoa. Wokovu ni uhalisia wa Yesu kurejesha sheria yake hai ya upendo ndani ya ubinadamu. Katika Warumi 3 tunasoma:

Lakini sasa Mungu ameifunua hali ya afya ya ndani—tabia iliyo sawa na kamilifu kwa kila njia—ambayo haikutokana na maandiko ya kisheria, bali ndiyo ile ambayo Maandiko na Amri Kumi zilikuwa zikielekeza akili zenu. Hali hii kamilifu hutoka kwa Kristo na huumbwa ndani yetu na Mungu tunapomwamini. Uaminifu wetu kwake huanzishwa kwa ushahidi uliotolewa kupitia Yesu Kristo wa uaminifu wake wa juu kabisa. Hakuna tofauti kati ya makabila, kwa maana wanadamu wote wameambukizwa ugonjwa ule ule—wa kutoamini, hofu, na ubinafsi—na wamepotoshwa katika tabia na kukosa sana kiwango cha utukufu wa Mungu kwa ubinadamu. Hata hivyo, wote walio tayari huponywa bure kwa Dawa ya neema ya Mungu iliyotolewa na Yesu Kristo. Mungu alimtoa Yesu kama njia na chombo cha urejesho. Sasa, kupitia uaminifu uliowekwa kwa ushahidi wa tabia ya Mungu uliofunuliwa Kristo alipokufa, tunaweza kushiriki Dawa hiyo iliyopatikana kwa njia ya Kristo. Mungu alifanya hivi kuonyesha kwamba yeye ni wa haki na mwema—kwa maana kwa uvumilivu wake alisimamisha kwa muda matokeo ya mwisho ya kutokuwa katika upatanifu na muundo wake wa maisha—ingawa ameshtakiwa kwa uongo kuwa si wa haki. Alifanya hivi kuonyesha kwa wakati huu jinsi alivyo wa haki na mwema, ili aonekane kuwa wa haki anapowaponya wanaomwamini Yesu. (Warumi 3:21–26 Remedy).

Paulo anaendelea na hoja hii katika Warumi, lakini tukiruka hadi sura ya 14, anahitimisha tatizo kuu la dhambi:

Kila kisichotokana na imani ni dhambi (Warumi 14:23 NIV).

Hili ndilo tatizo, swali husika, kiini cha wokovu. Kwa msingi wake, dhambi ni kutomwamini Mungu. Adamu na Hawa walimkosa Mungu kwa kutoamini, na kutoamini kwao kulibadilisha roho yao kutoka upendo na uaminifu kwenda hofu na ubinafsi. Hofu na ubinafsi husababisha watu kutenda ili kujilinda na kujikuza—ambayo ni kinyume cha upendo.

Kwa sababu ya dhambi ya Adamu, tunazaliwa na roho ya hofu na ubinafsi, na wokovu unahitaji tuzaliwe upya kwa Roho/uzima wa Yesu—roho ya upendo na uaminifu. Hili haliwezi kutimizwa kwa sheria zilizowekwa kwa nguvu na utekelezaji wake. Kwa kweli, sheria zilizowekwa kwa nguvu huongeza hofu na kupunguza uaminifu na upendo. Uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi kama sheria za kibinadamu husababisha dini za kisheria kama ile ya Wayahudi waliomsulubisha Kristo; lakini wokovu unahitaji kuzaliwa upya.

Utii anaoutamani Mungu si kufanana kwa tabia ya kutunza kanuni, bali ni utii wa marafiki wanaopenda, mioyo yao imebadilishwa kutoka kutoamini, hofu, na ubinafsi kwenda ukweli, upendo, na uaminifu. Hili hutimizwa tu kwa njia za Mungu za ukweli na upendo; ndiyo maana Biblia inasema:

“Si kwa nguvu wala kwa uwezo, bali kwa Roho yangu,” asema BWANA wa majeshi (Zekaria 4:6 NIV).

Mungu hawezi kushinda, wala kurejesha upendo na uaminifu mioyoni na akilini kwa kutumia nguvu na uwezo; hufanya hivyo kwa Roho wake wa ukweli na upendo.

Utii wa kweli ni utii unaochipuka kutoka kwa upendo na uaminifu kwa Mungu, unaotoka katika moyo uliozaliwa upya na unaochochewa na Roho wa Kristo.

Nakuhimiza ukatae uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi kama sheria za kibinadamu, na urejee kumwabudu Mungu kama Muumba, ukitambua kwamba sheria zote za Mungu ni sheria za ubunifu wa uumbaji zilizojengwa ndani ya jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Kisha, kama bado hujafanya hivyo, fungua moyo wako kwake na uzaliwe upya katika uzima tele ambamo utii wa kweli unawezekana—utiifu wa upendo na uaminifu!

 

 

Donate online, securely via PayPal using your credit or debit card (no PayPal account needed, unless you want to set up a monthly, recurring payment).


cancel recurring payment

 

Want to use zelle instead?
See how on our
Support and Donations page.

Upcoming Events

calendar

Testimonial Post Slider

Testimony 45

I have been confused for years about what [christianity] calls [its] most disgusting teaching. It has never made much sense to me and for that reason has been evermore empty. I have listened to your class off and on and have struggled determining what is truth, because of the resistance design law encounters in the church. So, I thank God for your ministry. What you teach makes sense. It’s logical and backed up by the power of love. I have never seen that in Christ until now. I am astounded by the insight that is found when we look at God’s ministry through design law. All strength to this message, as I believe it to be the power of God.

Brendon S.

 

Testimony 24

I wanted to thank you very much for presenting your understanding of God. I’ve always been troubled by this question: Why did Jesus have to die? Since my conversion I understood that The Father & Jesus are one, I did not have issues with that. But was there not any other way to save us than for Jesus to die? I guess I actually had a question about God – if He is so wise, how come He did not find another way? I did not see the real ‘beauty’  in the cross. Only when you explained the picture in the medical context, Jesus providing medicine for my selfishness, have I started to finally ‘see the light’. Thank you so much. Your seminar, “Healing the Mind,” are absolutely marvelous & have shared them with my family and many other people, including colleagues at work. Thanks, thanks, thanks. May God bless you abundantly in your ministry.

M. W., Australia

 

Testimony 57

You have helped make sense of thirty two years of confusion. The material you freely provide reorganized so much of my life into such a beautiful pattern that has always been hinted at from within, but misguided with my training and what I was experiencing externally. My filipno parents, who were converted from Catholicism to SDA, were sincere and did their best to raise me the right way and I have deep respect for them. However, being immigrants and not understanding the language made for a difficult transition as I was growing up, which also applied to my spiritual growth as I learned the patterns of religion. I have been listening to as many bible study classes and reading blog posts as my time in a work truck will allow, searching for the practical applications of where spirituality and reality meet, and I thank you for helping me find that. You have helped me reach a point in which I can truly say that I love God, that I believe He loves me, and, like David, I delight in His law. God bless.

Emmanuel V., Calgary, AB Canada

Testimony 27

Your teachings about our heavenly Father have changed my life. Thank you sooooooo very very much! I know He’s doing some serious healing in my heart and life and I look forward to each new day to learn something new about Him and to just hear you speak about Him. Thank you, forever.

Nancy S.

 

Testimony 62

I would like to express my thanks to the C&R team for creating a platform from which people can learn to trust in God and grow. My life is a witness to the effectiveness of this ministry. Without believing the truth about God as you have shown, I don’t know what my life would be like. I had given up on God helping me with certain sins – it was all useless. Given that the scripture is clear and God is so good, how could I have betrayed him so many times? I was a yo-yo christian; spinning up and down. My faith and enthusiasm was driven by discoveries/threats that prophecy is about to be fulfilled. But when I watched your “Healing the Mind” seminar, it was like a light finally went on. I could see God had no plan to hurt me, the danger came from sin, and that He is working to protect me and strengthen me. Thank you for allowing God to use you. The message God gave C&R saved my life!

Antony N. – Hobart, Australia

 

Testimony 9

I really enjoy with you the view of a gracious God. Thank you for sharing the work you are allowing the Lord to do in you.

L., Queensland, Australia

 

Testimony 74

Thank you so much for opening my eyes. I’ve been through a lot of ministries that just didn’t show the love of God that I felt he was. You have helped me to begin the process of true healing. I thought I was “too far gone,” now I know there’s hope in Jesus, because he loves us beyond what we can comprehend. Thank you again for all you do. I truly appreciate it and pray more people find you (physical at your studio and through this website).

Dalio M.

Testimony 32

The message [of Come And Reason Ministries is] for all Christians (and those who may become Christians) and not just Adventists or any other group. It is difficult to imagine why any [anyone] with intellectual and spiritual honesty could find fault with the way you explained the healing substitution concepts and the truth about God’s character, though I know some will reject and criticize. On behalf of those in our group near Tacoma, WA, thank you and your staff for all of the hard work and for sharing the Gospel in this manner. God’s message of healing love will be carried to the whole world and then Jesus will come – He promised it.

Terry U., Tacoma, WA, USA

 

Testimony 29

Thank you for all of your work to correct misconceptions about God’s character. So many people that my husband and I have talked to seem to be against the natural law construct and view it as “errant” and “dangerous.” Having learned more about it through your blogs and lessons, I don’t really understand why they view it that way, except that it means they have to relearn theology they have known for their entire lives. But I’m so excited to relearn this. For the past few years I have been questioning how I could trust a God who punishes arbitrarily and is full of wrath for those who don’t obey His commands. That view made me afraid to “mess up” or “not be good enough,” even within my relationship with God. I really appreciated the point you bring out about God not wanting us to serve Him because we are afraid, but because we love Him.

Melissa H., IN, USA

 

Testimony 3

My husband is a pastor and I listen to your lesson almost every week. Thank you for helping me in my study life and to help me love the “real” God more.

C. F., NC, USA

 

Testimony 34

I was introduced to Come and Reason Ministries by accident, via a passing comment made in a bible study class we were visiting. I checked this website out and my life was changed. The understanding of the truth of God’s character, and how we apply it, is so right. The tricky part is consistently applying which “lens” to look through. As I began to understand, I started sharing the basics of this understanding with a discussion group I was leading and, suddenly, a lot of things started to make sense that never used to. At the same time, I enjoyed an amazing opportunity. I was able to conduct a full bible study at WORK! What an amazing experience! It is such a joy to share the truth about God and to share how it all fits in the war between God and Satan. So many people benefit when we have a correct understanding about how God works and who He really is! Thank you for this transformational understanding. Keep up the good work! God Bless you!

Tony P., CA, USA

 

Testimony 40

I was brought up in a different faith and have been petrified my whole life of God. I believed that I would burn in hell for eternity. When I was 12 I started pursuing the things of this world, but for the next 45 years the Spirit was always calling me, as I knew there was a God through nature. I could see the vast sea of stars in the universe and knew there was something bigger out there. Five years ago, through a Revelation seminar, I was blessed to learn about God’s character and government.

Then I found Come and Reason Ministries and have come under some extreme pressure when I speak about the ministry. One time a member sent me an internet article titled “Whats wrong with Tim Jennings?” I asked her what she thought of it and she said “I don’t know, I didn’t read it.”

I have always wanted to find out for myself the truth about God, so I stayed with the Design Law construct and have been liberated to understand the big picture. Once we consider Design Law, all other Bible stories and prophecies seem to fit perfectly. It is truly beautiful to see people grasping how God operates this Universe of Love and the liberation it has provided in their lives. It blows my mind to see how consistent Design law is with what our founders believed. I hear statements like “This makes so much sense.”

Tom W., Mt. Pleasant, MI, USA

 

Testimony 22

I have found your Bible study class lectures to be very inspiring and useful as I prepare to teach class every other week. I subscribe to the podcast and download your notes on the weeks I teach. The audio and notes are such a great help in preparing. My own understanding of God’s character has grown as I teach the class. Commendations on the thought-provoking and well-prepared material Come and Reason provides. Personally, I get excited by the tie you make between the spiritual and mental/physical domains.

A.A. Corrales, NM, USA

 

Testimony 49

I came into the church at 21, but that is as far as it went. I was so confused about what love is. I couldn’t find it in the bible, because I am not a person that can read between the lines. I have no logic. I have read many, many books; trying to figure out the crux of the matter. They were helpful, but something was still missing. I have become very frustrated to the point of crying out to God, “Where can I go?”  I needed some basics.

I found two books, written by Timothy Jennings, MD, to be very helpful. God showed me that I had lived my whole life in fear. I didn’t even see it. Now, I do. God is so good.  I discovered the “The Remedy”  Dr. Jennings new book, “The God-Shaped Heart!” Oh, I was so excited, I purchased them right away.

I can get rid of most of my books, because “The Remedy” brings the Love of God out so clearly, even I can’t miss it. Now, I want to sit and read my Bible. Wow, what a revelation! It is just simply Awesome! I am so grateful to Jehovah Almighty for hearing my prayer for more understanding! I am so encouraged!

Jackie S.

 

Testimony 66

I am incredibly grateful for the transformative impact you’ve had on my life, and words cannot fully express my appreciation. Over the years, I have been an avid listener and follower of C&R and extend my heartfelt thanks for creating the C&R mobile app. It has allowed me to immerse myself in your lessons repeatedly, enabling me to grasp the profound significance about the Character of God, Design Law, the protocols for life, the reasons behind the current chaos, and Christ’s mission to restore everything. They have deeply touched me. Having studied with various churches, I came away with the perception that God is no different from the deities of ancient Greek or Roman mythology—demanding sacrifices and taking pleasure in bloodshed. Thanks to your transformative teachings, I have experienced a profound awakening to the true nature of God and the immense power of His love. It is truly a remarkable and liberating sensation to finally grasp the truth and embrace the empowering nature of God’s laws. My self-perception has become brighter and more infused with love. My journey of growth continues on a daily basis.

Chris P., Lake Mary, FL, USA