Call Us: 423 661-4734 | Email: requests@comeandreason.com      
JE, NI UTII WA IMANI AU WA SHERIA?

JE, NI UTII WA IMANI AU WA SHERIA?

Wana wa Israeli walipokaribia mwisho wa miaka yao 40 ya kutangatanga jangwani na walipokuwa karibu kuingia Kanaani, Yoshua aliyekuwa akiwaongoza alipokea ujumbe ufuatao kutoka kwa Mungu:

Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda kulingana na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kulia, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako. (Yoshua 1:7).

Unaelewaje maagizo haya? Unaposikia mwito wa kutii sheria ya Mungu, nini huja akilini mwako? Je, unafikiria sheria ya Mungu kama sheria za kibinadamu — kanuni zinazowekwa ambazo Mungu huzisimamia na kutekeleza kwa adhabu? Au unafikiria sheria ambazo Muumba aliweka katika utendaji wa uhalisia — sheria za fizikia, mvuto (gravity) , afya, na sheria za maadili?

Je, unasikia mwito wa Mungu wa utii kama vile mwito wa daktari wa kuishi kwa afya (katika mwafaka na sheria za afya), au unasikia mwito wa Mungu wa utii kama onyo la askari polisi la kutokukimbiza gari kwa mwendo kasi?

Ni ukweli wa kusikitisha wa historia kwamba sehemu kubwa ya Ukristo imekubali uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi sawa tu na sheria za wanadamu—kanuni zilizobuniwa na kutekelezwa kwa adhabu. Lakini hebu tuchunguze utii unaotokana na sheria, kanuni, vitisho vya adhabu, na utekelezaji wa sheria—ukilinganisha na utii unaotokana na upendo, uaminifu, ambao pia hujulikana kama imani. Kisha tuchunguze jinsi upendo na uaminifu vinavyopandwa katika mioyo na akili na kupelekea utii.

 

UTII WA SHERIA

Fikiria umesimama chini ya msalaba wakati Yesu anasulubiwa. Unazungumza na Kayafa na viongozi wengine wa dini ya Kiyahudi wanaomdhihaki, kumtesa, na kumsulubisha Kristo. Unadhani wangetoa majibu gani kwa maswali yafuatayo?

  • Je, ni muhimu kuwa na utii wa agano kwa Mungu? “Kabisa!” naweza kuwasikia wakisema, “Tunaishi kwa ili kutii agano—sisi sote tumetahiriwa ipasavyo kama agano linavyoagiza.”
  • Je, ni muhimu kuitii sheria ya Mungu? “Bila shaka. Na kama hawa wahalifu hawatakufa upesi, tutamwomba Pilato aharakishe vifo vyao ili tuweze kuitunza Sabato kulingana na sheria.”
  • Je, ni muhimu kuitii sheria ambayo Musa mtumishi wa Mungu alitupa? “Bila shaka! Maisha yetu yote tunaishi tukilenga kutii sheria hiyo.”

Na kama tungewauliza, “Kwa nini mnamsulubisha huyu mtu?” naweza kuwasikia wakijibu:

“Naam, umeshatueleza wewe mwenyewe—lazima tuwe watiifu kwa agano, lazima tutii sheria ya Mungu, lazima tutii sheria ambazo Mungu alitupatia kupitia Musa—na huyu mtu anazivunja mara kwa mara. Musa alituagiza tumpige kwa mawe mzinzi, lakini huyu mtu aliwasamehe. Musa alitupa ruhusa ya kuwataliki wake zetu, lakini huyu mtu alisema tusifanye hivyo. Musa alitufundisha tusifanye kazi siku ya Sabato, lakini huyu mtu aliwaponya wagonjwa siku ya Sabato na wanafunzi wake walivuna punje siku ya Sabato. Musa alitufundisha kuosha kwa namna fulani kabla ya kula, lakini huyu mtu hakuwaelekeza wanafunzi wake wafanye hivyo. Musa alitufundisha kwamba sheria lazima zitekelezwe na kwamba uovu lazima uondolewe katika jamii, na ndicho tunachofanya kwa sababu sisi ni watoto wa Abrahamu na wa Mungu, na tumejitoa kwa uaminifu na utii wa agano.”

Utii wa sheria na utekelezaji wa sheria hauna uwezo wa kubadili mioyo na akili, wala kusimika upendo, uaminifu, urafiki, uaminifu wa kudumu, na kujitoa. Utii wa uongozi wa Kiyahudi uliomsulubisha Kristo ulikuwa aina iliyowafanya wawe maadui wa Mungu huku wakidai kuwa watoto wake na kufanya kazi yake.

Mtume Paulo anashughulikia mwelekeo huu wote wa kisheria usio sahihi kuhusu utii katika kitabu cha Warumi, na analinganisha utii unaotokana na sheria na utii unaotokana na imani au uaminifu. Anaanza kitabu cha Warumi kwa kusema:

Kupitia yeye na kwa ajili ya jina lake, tumepokea neema na utume ili kuwaita watu kutoka mataifa yote katika utii unaotokana na imani. (Warumi 1:5).

Imani au uaminifu si kitu kinachoweza kuamriwa, kutungwa kwa sheria, kuagizwa, au kupatikana kwa njia ya sheria na utekelezaji wake. Uaminifu hujengwa juu ya uaminifu halisi wa maisha, unaohitaji ushahidi, ambao lazima ueleweke na kuishiwa. Uaminifu hauwezi kuanzishwa kwa tangazo, madai, amri, maagizo, kanuni, na masharti, na utadhoofishwa na vitisho na adhabu. Jaribu kupata uaminifu wa mtu kwa kumtishia kumdhuru au kumwadhibu ikiwa hatakuamini—haiwezekani kabisa! Sheria zilizolazimishwa na utekelezaji wake haziwezi kuvutia mioyo na akili, na hatimaye, zitawageuza wale wanaotumia mbinu hizo kama njia ya kutafuta haki kuwa waasi.

Paulo, akielewa hili, baada ya kutufundisha kwamba anawaita watu kwenye utii unaotokana na imani, anatueleza msingi wa imani hiyo. Katika Warumi 1:20 anaandika:

Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, sifa zisizoonekana za Mungu—uwezo wake wa milele na asili yake ya uungu—zimeonekana wazi, zikieleweka kutokana na mambo yaliyoumbwa, hivyo watu hawana udhuru (NIV msisitizo wangu).

Imani yetu kwa Mungu haijengwi juu ya madai, maneno, au amri, bali juu ya uhalisia, ushahidi, na ukweli. Mungu ni Muumba, na sheria zake ndizo sheria zinazoongoza jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Paulo anatufahamisha kwamba ufalme wa Mungu ni ufalme wa uhalisia—sheria za milele za muundo (design laws) zinazoongoza shughuli za asili—na kwa hiyo ufalme wa Mungu haufanyi kazi kwa kanuni zilizobuniwa zinazohitaji adhabu za nje kama viumbe hufanya.

Paulo anaendelea kusema kwamba watu ambao hawajaletewa Neno la Mungu lililoandikwa, lakini wanaelewa uhalisia wa ufalme wa Mungu wa ukweli, upendo, na uhuru unaofunuliwa kupitia sheria za ubunifu wa uumbaji zilizojengwa katika asili, na hivyo kuchagua kumwamini, hupokea moyo mpya na roho iliyo sahihi, na sheria ya Mungu huandikwa mioyoni mwao. Wanakuwa washiriki wa agano jipya la wokovu (Waebrania 8:10).

“Wote watendao dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, na wote watendao dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria [Torati]. Kwa maana si wale wanaosikia sheria ndio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaotii sheria atakaotangazwa kuwa wenye haki. (Hakika, watu wa mataifa, wasio na sheria, wanafanya kwa asili mambo yanayotakiwa na sheria, wao wenyewe ni sheria kwao, ingawa hawana sheria, kwa kuwa wanaonyesha kwamba matakwa ya sheria yameandikwa mioyoni mwao, dhamiri zao zikiwa mashahidi, na mawazo yao mara nyingine yakiwashitaki, mara nyingine hata yakiwatetea.)” (Warumi 2:12–15, NIV84, msisitizo wangu).

Paulo anaeleza uhalisia kwamba sheria za ubunifu wa Mungu zimejengwa ndani ya jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Hata kama hakuna mtu anayekufundisha shuleni, wala husomi katika kitabu, lakini unazitambua katika asili na kuishi kwa upatanifu nazo kwa sababu unazithamini na kuzichagua, basi umechagua kumwamini Muumba, na Roho Mtakatifu hufanya kazi moyoni mwako kuandika sheria yake ndani yako. Kupitia ushindi wa Kristo, Roho Mtakatifu huleta maisha ya Kristo—ya ukweli, upendo, na uhuru—sheria za ubunifu wa Mungu—na kuzizalisha katika akili na moyo wako; huo ndio uzoefu wa agano jipya. Hata kama mtu bado hajasikia jina la Yesu, bado anaokolewa naye kwa sababu Yeye ni Muumba na Mtegemezaji wa asili. Uponyaji huu, mabadiliko, urejesho wa moyo na akili hauwezi kufanywa kwa njia za kisheria za nje.

Kuwa makini na kile Paulo anaandika baadaye:

Basi wewe unayejiita Myahudi; unayelitegemea torati na kujisifu kwa uhusiano wako na Mungu; unayejua mapenzi yake na kuidhinisha yaliyo bora kwa kuwa umefundishwa na torati; unayejiaminisha kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, nuru kwa walio gizani, mwalimu wa wapumbavu, mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una umbo la maarifa na ukweli katika torati—wewe basi unayefundisha wengine, hujifundishi? Wewe uhubiriye usiibe, waiba? Wewe usemaye watu wasizini, wazini? Wewe uchukiaye sanamu, waibia mahekalu? Wewe ujisifuye kwa torati, wamheshimu Mungu kwa kuivunja torati? Kama ilivyoandikwa: “Jina la Mungu linakufuriwa kati ya Mataifa kwa sababu yenu.” (Warumi 2:17–24 NIV).

Paulo anakabiliana na njia ya utii inayotegemea sheria zilizowekwa kwa nguvu, dini ya kisheria, na kutunza kanuni. Hii ni sawa na kuwaambia madaktari:

“Enyi mnaojiita viongozi wa huduma ya afya, mnaotegemea maarifa ya vitabu vyenu vya udaktari na kujisifu kwamba mna elimu zaidi; mkijiona kuwa waongoza wagonjwa kwa sababu mna vitabu—mbona hamjifundishi kuishi kwa afya? Kwa nini hamwachi kuvuta sigara? Kwa nini hamwachi kunywa pombe? Kwa nini hampati saa nane za usingizi kila usiku? Ninyi mnaochukia magonjwa kwa wengine na kujisifu kwa utaalamu wenu, kwa nini mnamdharau Mungu kwa kuvunja sheria zake za afya kwa jinsi mnavyoishi? Kama ilivyoandikwa, Mungu anawakilishwa vibaya kwa sababu yenu.”

Baada ya Paulo kuwaonya kwa kuwa na mtazamo wa kisheria wa dini huku wakiishi kinyume na sheria za ubunifu was Mungu katka uumbaji, anaandika:

Kwa kweli, Mataifa wasiotahiriwa wanaoitunza sheria ya Mungu watawahukumu ninyi Wayahudi mliotahiriwa na mnao torati lakini hamtiii (Warumi 2:27 NLT).

Paulo anasema kwamba wale ambao hawajawahi kwenda shule ya udaktari lakini wanaishi kwa upatanifu na sheria za afya za Mungu watawahukumu madaktari walio na vitabu lakini wanavunja sheria za afya.

Kisha anaeleza kwamba tohara si ya kisheria, ya tabia, au ya nje, bali ni tohara ya moyo kwa Roho—uhalisia—kukata roho ya hofu na ubinafsi na kuanzisha utambulisho wetu juu ya Roho Mtakatifu wa Mungu – maisha ya Kristo, roho ya upendo na uaminifu, inayoturejesha katika upatanifu na sheria za muundo za Mungu kwa maisha.

Paulo anaendelea kusisitiza kwamba sheria zilizowekwa kwa nguvu, dini ya kisheria, na utendaji wa nje havina nguvu ya kuokoa. Wokovu ni uhalisia wa Yesu kurejesha sheria yake hai ya upendo ndani ya ubinadamu. Katika Warumi 3 tunasoma:

Lakini sasa Mungu ameifunua hali ya afya ya ndani—tabia iliyo sawa na kamilifu kwa kila njia—ambayo haikutokana na maandiko ya kisheria, bali ndiyo ile ambayo Maandiko na Amri Kumi zilikuwa zikielekeza akili zenu. Hali hii kamilifu hutoka kwa Kristo na huumbwa ndani yetu na Mungu tunapomwamini. Uaminifu wetu kwake huanzishwa kwa ushahidi uliotolewa kupitia Yesu Kristo wa uaminifu wake wa juu kabisa. Hakuna tofauti kati ya makabila, kwa maana wanadamu wote wameambukizwa ugonjwa ule ule—wa kutoamini, hofu, na ubinafsi—na wamepotoshwa katika tabia na kukosa sana kiwango cha utukufu wa Mungu kwa ubinadamu. Hata hivyo, wote walio tayari huponywa bure kwa Dawa ya neema ya Mungu iliyotolewa na Yesu Kristo. Mungu alimtoa Yesu kama njia na chombo cha urejesho. Sasa, kupitia uaminifu uliowekwa kwa ushahidi wa tabia ya Mungu uliofunuliwa Kristo alipokufa, tunaweza kushiriki Dawa hiyo iliyopatikana kwa njia ya Kristo. Mungu alifanya hivi kuonyesha kwamba yeye ni wa haki na mwema—kwa maana kwa uvumilivu wake alisimamisha kwa muda matokeo ya mwisho ya kutokuwa katika upatanifu na muundo wake wa maisha—ingawa ameshtakiwa kwa uongo kuwa si wa haki. Alifanya hivi kuonyesha kwa wakati huu jinsi alivyo wa haki na mwema, ili aonekane kuwa wa haki anapowaponya wanaomwamini Yesu. (Warumi 3:21–26 Remedy).

Paulo anaendelea na hoja hii katika Warumi, lakini tukiruka hadi sura ya 14, anahitimisha tatizo kuu la dhambi:

Kila kisichotokana na imani ni dhambi (Warumi 14:23 NIV).

Hili ndilo tatizo, swali husika, kiini cha wokovu. Kwa msingi wake, dhambi ni kutomwamini Mungu. Adamu na Hawa walimkosa Mungu kwa kutoamini, na kutoamini kwao kulibadilisha roho yao kutoka upendo na uaminifu kwenda hofu na ubinafsi. Hofu na ubinafsi husababisha watu kutenda ili kujilinda na kujikuza—ambayo ni kinyume cha upendo.

Kwa sababu ya dhambi ya Adamu, tunazaliwa na roho ya hofu na ubinafsi, na wokovu unahitaji tuzaliwe upya kwa Roho/uzima wa Yesu—roho ya upendo na uaminifu. Hili haliwezi kutimizwa kwa sheria zilizowekwa kwa nguvu na utekelezaji wake. Kwa kweli, sheria zilizowekwa kwa nguvu huongeza hofu na kupunguza uaminifu na upendo. Uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi kama sheria za kibinadamu husababisha dini za kisheria kama ile ya Wayahudi waliomsulubisha Kristo; lakini wokovu unahitaji kuzaliwa upya.

Utii anaoutamani Mungu si kufanana kwa tabia ya kutunza kanuni, bali ni utii wa marafiki wanaopenda, mioyo yao imebadilishwa kutoka kutoamini, hofu, na ubinafsi kwenda ukweli, upendo, na uaminifu. Hili hutimizwa tu kwa njia za Mungu za ukweli na upendo; ndiyo maana Biblia inasema:

“Si kwa nguvu wala kwa uwezo, bali kwa Roho yangu,” asema BWANA wa majeshi (Zekaria 4:6 NIV).

Mungu hawezi kushinda, wala kurejesha upendo na uaminifu mioyoni na akilini kwa kutumia nguvu na uwezo; hufanya hivyo kwa Roho wake wa ukweli na upendo.

Utii wa kweli ni utii unaochipuka kutoka kwa upendo na uaminifu kwa Mungu, unaotoka katika moyo uliozaliwa upya na unaochochewa na Roho wa Kristo.

Nakuhimiza ukatae uongo kwamba sheria ya Mungu hufanya kazi kama sheria za kibinadamu, na urejee kumwabudu Mungu kama Muumba, ukitambua kwamba sheria zote za Mungu ni sheria za ubunifu wa uumbaji zilizojengwa ndani ya jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Kisha, kama bado hujafanya hivyo, fungua moyo wako kwake na uzaliwe upya katika uzima tele ambamo utii wa kweli unawezekana—utiifu wa upendo na uaminifu!

 

 

Donate online, securely via PayPal using your credit or debit card (no PayPal account needed, unless you want to set up a monthly, recurring payment).


cancel recurring payment

 

Want to use zelle instead?
See how on our
Support and Donations page.

Upcoming Events

calendar

Testimonial Post Slider

Testimony 49

I came into the church at 21, but that is as far as it went. I was so confused about what love is. I couldn’t find it in the bible, because I am not a person that can read between the lines. I have no logic. I have read many, many books; trying to figure out the crux of the matter. They were helpful, but something was still missing. I have become very frustrated to the point of crying out to God, “Where can I go?”  I needed some basics.

I found two books, written by Timothy Jennings, MD, to be very helpful. God showed me that I had lived my whole life in fear. I didn’t even see it. Now, I do. God is so good.  I discovered the “The Remedy”  Dr. Jennings new book, “The God-Shaped Heart!” Oh, I was so excited, I purchased them right away.

I can get rid of most of my books, because “The Remedy” brings the Love of God out so clearly, even I can’t miss it. Now, I want to sit and read my Bible. Wow, what a revelation! It is just simply Awesome! I am so grateful to Jehovah Almighty for hearing my prayer for more understanding! I am so encouraged!

Jackie S.

 

Testimony 16

Your seminars are still inspiring and changing our lives and we continue to share the principles we have learned from you. Your ministry has changed our lives!

E.W.

 

Testimony 1

Thank you! I love listening to the Come And Reason Ministries Bible study classes and am using some of your notes to get the lessons together that I will be teaching. You always have such good quotes and Bible texts and pull things together to make good sense.

T. C., IN, USA

 

Testimony 46

Over the past couple of years God has been expanding my view of Himself and His character. Along my approximately 40-year journey, I have often had questions, but was hesitant to voice these and step outside the traditionally accepted thinking, for fear of admitting that I may in fact be eternally lost. In the recesses of my thinking has been the thought – if one blindly accepts (which is widely regarded as “real faith”) and does not question, is this really ‘truth?’ I often find it challenging to grapple with very theological ‘speak,’ but Dr. Jennings has a real gift of explaining spiritual concepts with clear practical examples. The weekly discussions are growing my Christian experience and slowly changing my view of how to live as a child of God in today’s complex world. Finally the whole Old Testament sanctuary teaching moved in my mind from fantasy to reality!

Beverly S., South Africa

 

Testimony 8

Thank you for the ministry you are sharing with us, it is a real blessing to us and especially to my husband and myself! You are encouraging us to think for ourselves and not just to except everything, without thinking it through, with God’s word!

M.K., USA

 

Testimony 31

It was very touching to hear the testimony of your class share how viewing God’s true character has changed their lives. My feelings are the same – there is so much freedom in knowing that God LOVES me – regardless of my… just, REGARDLESS! I’m still blown away by the true gospel, the fact that God is not ready to strike us when we fail. He is not arbitrary. He simply loves us and warns of the natural consequences because He can’t stand to see us suffer. I AM IN LOVE WITH THIS GOD!!!

Ceil V.,  UT, USA

 

Testimony 63

I’ve been very blessed by “The God Shaped Brain” and this ministry, through video and podcast, over the last few years. It’s truly opened up my eyes more to the truth about God and the importance of that truth in the present world. The message is so inviting, freeing and enlightening and MORE people need to know about it. I believe it is the last message that can truly, not only prepare a people for salvation and translation, but vindicate the character of God.

Michael V., Yonkers, NY, USA

 

Testimony 62

I would like to express my thanks to the C&R team for creating a platform from which people can learn to trust in God and grow. My life is a witness to the effectiveness of this ministry. Without believing the truth about God as you have shown, I don’t know what my life would be like. I had given up on God helping me with certain sins – it was all useless. Given that the scripture is clear and God is so good, how could I have betrayed him so many times? I was a yo-yo christian; spinning up and down. My faith and enthusiasm was driven by discoveries/threats that prophecy is about to be fulfilled. But when I watched your “Healing the Mind” seminar, it was like a light finally went on. I could see God had no plan to hurt me, the danger came from sin, and that He is working to protect me and strengthen me. Thank you for allowing God to use you. The message God gave C&R saved my life!

Antony N. – Hobart, Australia

 

Testimony 66

I am incredibly grateful for the transformative impact you’ve had on my life, and words cannot fully express my appreciation. Over the years, I have been an avid listener and follower of C&R and extend my heartfelt thanks for creating the C&R mobile app. It has allowed me to immerse myself in your lessons repeatedly, enabling me to grasp the profound significance about the Character of God, Design Law, the protocols for life, the reasons behind the current chaos, and Christ’s mission to restore everything. They have deeply touched me. Having studied with various churches, I came away with the perception that God is no different from the deities of ancient Greek or Roman mythology—demanding sacrifices and taking pleasure in bloodshed. Thanks to your transformative teachings, I have experienced a profound awakening to the true nature of God and the immense power of His love. It is truly a remarkable and liberating sensation to finally grasp the truth and embrace the empowering nature of God’s laws. My self-perception has become brighter and more infused with love. My journey of growth continues on a daily basis.

Chris P., Lake Mary, FL, USA

 

Testimony 56

I cannot thank you enough for opening my understanding to the beautiful truth of God’s Law of Love and how it applies to everything. I have been a Christian for over forty years, but I feel like I am only now seeing with my eyes open. Thank you, Thank you, Thank you!!

Tammy Cinzio, Australia

 

Testimony 61

I grew up in a prominent protestant church and had what I like to call religious anxiety. I’ve always had questions about God and Salvation that no one could seem to answer.  I didn’t know how to find resolution. During 2020, at the height of my anxiety, I fell to my knees and begged God to show me truth and light and to give me the hope that I’ve been longing for. Days later, I stumbled upon your online videos and it was like a veil was lifted and EVERYTHING made sense! For the first time in my almost 39 years of life, my religious/spiritual anxiety has lessened. I feel a sense of freedom and peace I’ve NEVER had before… and it’s all because my view of God has changed. Thank you!

Ashleighn C.

 

Testimony 50

After coming into contact with Come And Reason Ministries, I can finally say that many of my unanswered questions have fallen into place. I discovered that my view of God’s Law was “imposed laws and rules” with “imposed punishments” and that this was the major culprit of my many unanswered questions. Thanks be to God for using you and those around you to help us who have struggled with this “infection” of thought. I have now rejected the “imposed law” concept to fully embrace “Design Law”… to look thru “Design Law,” instead of “imposed law,” is a relief.

Viliami L., Australia

 

Testimony 53

I was so blessed by a friend who gave me your book, “The God Shaped Brain,” while I was sitting in church asking God to please help me learn more about Him and help me not to be so confused and scared. That was about 2 years ago. Your books have helped me to love God even more. I’m not confused or scared anymore! I have listened to all of your bible study classes and feel like I know the wonderful people that attend every week. Thank you for all that you’re doing in spreading the true message about God and His law of love. God bless you and your whole class.

Elssy P., Modesto, CA, USA

 

Testimony 28

I have been following your Bible study class for about a year now. I must say I am impressed with how your ministry has grown. I took it upon myself to listen to all your lesson podcasts from the past and they have both enriched me physically, mentally, emotionally and spiritually. I have learnt a lot from this class. I have also noticed how the class has grown in spiritual strength. One of the things that benefited me is that now I am not afraid of God. I use to be, but now it has melted away. The second thing is that you helped me to have a real life relationship with God. Now He is my friend that was always there and I love having him with me all the time. Thirdly, because of this class, it inspired me to take over and lead a class. I have called it “Let Us Reason Together,” adapting your inquisitive style and creating a class of free thinkers.

T. Banda, Malawi, Africa

 

Testimony 64

I’ve been reading the bible and walking with Jesus since I was around 16. I’m 42 now. I’ve mostly been alone in my walk although I went to several churches in different denominations. For the past 3 years God has been showing me His character of agape. It’s been a blessing and changed how I view God and my walk with Jesus. About a year ago I came across the power of love and the principles of design law. These teachings changed how I read scripture and have been such a beautiful blessing. I’m very excited and grateful for these truths. We share these truths of agape, design law and the reality of the principles of the two trees in the garden of Eden with people on Facebook and YouTube. People all over are learning to trust God and His agape design law which makes life possible. Thank you for everything you shared with me. May God continue to bless your ministry and lives.

Bradley M., Hinsdale, NY, USA