Call Us: 423 661-4734 | Email: requests@comeandreason.com      
WATU WA NDANI, WATU WA NJE, NA MPANGO WA MUNGU KWA MAISHA

WATU WA NDANI, WATU WA NJE, NA MPANGO WA MUNGU KWA MAISHA

Hivi karibuni, msikilizaji mmoja mtandaoni alituma maswali yafuatayo:

Je, watu huwa aidha watu wa ndani au watu wa nje? Je, wewe ni mmoja kati ya hao? Yesu alikuwa nani kati ya hao? Je, unaweza kuwahudumia watu ikiwa wewe ni mtu wa ndani?

Katika miaka ya 1920, daktari wa akili Carl Jung alibuni maneno mtu wa ndani(introvert) na mtu wa nje (extrovert) ili kuelezea aina mbili za tabia. Mtu wa ndani hulenga nguvu zake za kiakili na hutegemea nafsi yake ili kujipatia upya na kujichangamsha, ilhali mtu wa nje hulenga nguvu zake nje na hupata hali ya kujipatia upya na kujichangamsha kupitia wengine.

Tangu wakati huo, mengi yameandikwa kuhusu mitindo hii miwili ya tabia, na aina zake ndogo nyingi pia zimeelezewa. Nadharia zimependekezwa kuhusu tofauti katika kazi za mizunguko ya ubongo, uzoefu wa maisha, mifumo ya mtiririko wa damu, kemia ya neva, vinasaba, na majibu yanayojifunzwa, lakini hakuna maelezo ya kibaolojia yaliyo kubalika kwa wote ambayo yamepatikana.

Lakini katika kutafuta ufahamu, muulizaji kwa hekima alimrejelea Yesu. Alijiuliza: Yesu alikuwa mtu wa ndani au mtu wa nje?

Yesu alikuwa mwanadamu mkamilifu na pia alikuwa udhihirisho wa Mungu. “Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake” (2 Wakorintho 5:19). Yesu alisema, “Mtu yeyote aliyeniona mimi amemwona Baba” (Yohana 14:9). Na Yesu ndiye Mungu aliyefanyika mwanadamu (Yohana 1:1–3, 14).

Yesu ni Mungu katika ubinadamu, na ndani ya Yesu tunaona utekelezaji, uhai, na dhihirisho la tabia ya Mungu ya upendo na ukweli. Upendo wa Yesu ulimfanya azingatie wengine, katika kuokoa, kuponya, kubariki, kuinua, na kumpea Baba yake utukufu. Hivyo basi, wakati upendo na ukweli vilipohitaji, Yesu alikuwa mtu wa nje katika kupeleka mbele ukweli na upendo (uponyaji wa hadhara, mahubiri, miujiza ya kuwalisha maelfu, n.k.); lakini wakati upendo na ukweli vilipomhitaji, Yesu alikuwa mtu wa ndani (kunyamaza, kuondoka kimya kimya, n.k.).

Yesu hakuwa mtu wa ndani kwa mujibu wa ufafanuzi wa Jung wa kujielekeza ndani ya nafsi yake ili kupata nguvu na kujichangamsha, wala hakujitenda kama mtu asiyeonekana. Vilevile hakuwa mtu wa nje kwa kutafuta nguvu na kujichangamsha kutoka kwa watu, wala hakujionyesha kama mtu wa sherehe anayependa kuwa kitovu cha furaha.

Badala yake, Yesu alikuwa dhihirisho kamili la mpango wa Mungu kwa ajili ya binadamu. Alitafuta nguvu na kujichangamsha kwa kuwa na muda na Baba yake, akimpenda Baba yake kwa moyo wake wote, akili zake zote, nafsi yake yote, na nguvu zake zote. Alijitenga na watu kwa muda ili kupata nguvu na kujichangamsha pamoja na Baba yake, kisha akatoka kuwahudumia wengine kwa ukweli na upendo wa Mungu, akitenda kama mtu wa nje katika hali zilizosaidia kuendeleza ufalme wa Mungu na akitenda kama mtu wa ndani katika hali zilizosaidia kuendeleza ufalme wa Mungu.

Yesu alikuwa udhihirisho wa upendo na ukweli uliomtukuza Baba na kuwabariki watu.

Katika ulimwengu huu wa dhambi, roho ya hofu na ubinafsi iliyo ndani ya mwanadamu humfanya atafute amani na faraja—kile kinachomfanya ajihisi salama zaidi. Watu wa ndani na watu wa nje, kama Jung alivyowafafanua, mara nyingi ni watu wasio na usalama wa ndani wanaojaribu kufidia hofu zao za ndani—hofu ya kukataliwa, upweke, kutotosheleza, hatia, na aibu—kupitia sura yao ya kuwa mtu wa ndani au wa nje.

Kwa maneno mengine, introvert anaweza kuwa anajitegemea kupita kiasi anaposhughulika na wengine, akachoka na kuchoshwa, kisha ajitenge ili kujichaji upya; au hujitenga ili kuepuka wasiwasi unaotokana na hofu ya kutotosheleza, hofu ya kufanya makosa, hofu ya watu watasemaje, aibu, n.k., na hivyo hujiondoa ili kuepuka umakini juu yake. Extrovert, kwa kuwa mchangamfu, mwenye sauti kubwa, mcheshi, na mwenye kuburudisha, mara nyingi hufanya hivyo akitafuta kukubalika na sifa kutoka kwa wengine ili kufidia hofu na kutokujiamini vilivyo ndani yake.

Yesu anawaita wote— introvert na extrovert—wamgeukie Yeye wawe conVERTS! Yesu anawasihi wote waache maisha ya hofu na ubinafsi tuliyorithi kutoka kwa Adamu, na wazaliwe upya wakiwa na roho mpya na moyo mpya, wakiwa na Roho wake wa upendo na uaminifu, na wasiishi tena wakitawaliwa na roho ya hofu. Na mioyo yetu ikizaliwa upya kwa roho ya upendo na uaminifu, hatutafuti tena nguvu kutoka kwetu wenyewe au kutoka kwa watu, bali kama Yesu, kila siku tunatumia muda pamoja na Yeye na Baba yetu wa mbinguni na kupata nguvu, uhai, msukumo, na motisha kutoka kwake. Kama Biblia inavyosema, upendo wa Kristo unatuchochea (2 Wakorintho 5:14).

Kwa moyo huu mpya wa upendo, na akili zetu zikiwa zimemwelekea Yesu badala ya nafsi zetu, tunatafuta kumtukuza Mungu kwa kutimiza makusudi yake katika maisha yetu. Kwa hiyo, tutatenda kwa namna ya mtu wa nje pale ambapo hilo linamtukuza Mungu na kuwabariki wengine, na tutatenda kwa namna ya mtu wa ndani pale tunapohitaji kunyamaza na hilo linamtukuza Mungu. Lakini msukumo wetu wa ndani hautakuwa tena hofu na kutokujiamini, bali upendo na uaminifu kwa Mungu—kwa utukufu wake na baraka ya wengine.

Hatimaye, usichanganye utu wa ndani na utu wa nje na vipawa—watu wengine wamepewa kipawa cha muziki, cha kuzungumza, na cha uongozi ambacho kitawaita katika majukumu yanayoonekana kwa namna ya “watu wa nje.” Wengine watapewa uwezo na talanta zinazofanya kazi kwa ufanisi zaidi nyuma ya pazia na kuonekana kama “watu wa ndani.” Lakini mtu ambaye si wa ndani wala wa nje, ambaye ni kama Yesu, atajikuta akifuata uongozi wa Roho Mtakatifu, na wakati hali ni kwamba ufalme wa Mungu unasonga mbele kwa ufanisi zaidi kupitia kimya, msemaji, mwanamuziki, au kiongozi atabaki kimya, au kama Yesu, ataondoka kimya kimya. Na wakati hali ni kwamba ufalme wa Mungu unasonga mbele kwa ufanisi zaidi, mtu ambaye kwa kawaida hutimiza majukumu yake nyuma ya pazia atasema kwa ujasiri akifuata msukumo wa Roho Mtakatifu.

 

 

 

Donate online, securely via PayPal using your credit or debit card (no PayPal account needed, unless you want to set up a monthly, recurring payment).


cancel recurring payment

 

Want to use zelle instead?
See how on our
Support and Donations page.

Upcoming Events

calendar

Testimonial Post Slider

Testimony 68

Your message of design law vs imperial law is so uplifting and makes so much sense- it is a game changer for me. The fact that Jesus’s death is not a big payment by an angry God is , quite frankly, a relief.

Laura G., London, Ontario, Canada

 

Testimony 12

I have been really blessed reading your response to the various questions on your site.

K.C., OH, USA

 

Testimony 1

Thank you! I love listening to the Come And Reason Ministries Bible study classes and am using some of your notes to get the lessons together that I will be teaching. You always have such good quotes and Bible texts and pull things together to make good sense.

T. C., IN, USA

 

Testimony 5

We listen to your bible studies lessons in our class in Montana. You actually were the main reason I decided to get a laptop, so I can go to your site and listen, read, learn, and print the class notes. I am so grateful to learn the correct view of God and his character. Now, to just have others have an interest in knowing, so I can share it with them. Good thoughts your way.

R. N., MT, USA

 

Testimony 44

We were given a gift of the DVD set, “God and Your Brain,” and we just finished watching it. The truths in this are so powerful and truly an answer to a prayer. We’re seeing hope where once we thought God wasn’t answering our prayers to be free of certain mindsets. He answered with these DVDs and we are hungry for more. Thank you!

Daniel T., Easley, SC, USA

 

Testimony 49

I came into the church at 21, but that is as far as it went. I was so confused about what love is. I couldn’t find it in the bible, because I am not a person that can read between the lines. I have no logic. I have read many, many books; trying to figure out the crux of the matter. They were helpful, but something was still missing. I have become very frustrated to the point of crying out to God, “Where can I go?”  I needed some basics.

I found two books, written by Timothy Jennings, MD, to be very helpful. God showed me that I had lived my whole life in fear. I didn’t even see it. Now, I do. God is so good.  I discovered the “The Remedy”  Dr. Jennings new book, “The God-Shaped Heart!” Oh, I was so excited, I purchased them right away.

I can get rid of most of my books, because “The Remedy” brings the Love of God out so clearly, even I can’t miss it. Now, I want to sit and read my Bible. Wow, what a revelation! It is just simply Awesome! I am so grateful to Jehovah Almighty for hearing my prayer for more understanding! I am so encouraged!

Jackie S.

 

Testimony 76

Warm greetings from Tanzania! I just wanted to take a moment to thank you and your team at Come And Reason Ministries for the amazing work you do. Your teachings have opened my eyes to deep biblical truths and how to live them out in real life. I started following the ministry back in 2018, and ever since, my walk with God has grown so much stronger. I’ve found freedom from fear-based faith and now live with more peace and trust in Him. I’ve also been sharing what I’ve learned, especially through Bible School discussions. Your lessons are so insightful and well-explained that I try not to miss a single one. May God continue to bless the work you’re doing.
Elisha M., Tanzania, Africa

Testimony 69

After reading your book, ‘Could It Be This Simple,’ someone was explaining Christianity in a way that made sense to me for the first time in my life. One morning, I simply prayed “I’m sorry and I love you.” As soon as I silently said that, I could literally feel God’s presence and light flood down on me from above and fill me up with love and joy. I sat there crying my eyes out, because I was so overpowered with this feeling of love and joy. It was just so incredible. I hope that more people can read this book and get a blessing from it. It’s really amazing.

Rachael H.

Testimony 57

You have helped make sense of thirty two years of confusion. The material you freely provide reorganized so much of my life into such a beautiful pattern that has always been hinted at from within, but misguided with my training and what I was experiencing externally. My filipno parents, who were converted from Catholicism to SDA, were sincere and did their best to raise me the right way and I have deep respect for them. However, being immigrants and not understanding the language made for a difficult transition as I was growing up, which also applied to my spiritual growth as I learned the patterns of religion. I have been listening to as many bible study classes and reading blog posts as my time in a work truck will allow, searching for the practical applications of where spirituality and reality meet, and I thank you for helping me find that. You have helped me reach a point in which I can truly say that I love God, that I believe He loves me, and, like David, I delight in His law. God bless.

Emmanuel V., Calgary, AB Canada

Testimony 16

Your seminars are still inspiring and changing our lives and we continue to share the principles we have learned from you. Your ministry has changed our lives!

E.W.

 

Testimony 13

I borrowed “Healing The Mind” DVDs from a friend and showed them at my home for a small gathering of women friends. Neither of my friends are Adventist, but they both enjoyed and embraced the messages you taught. In fact, one of the ladies prayed out loud in our group and that was the first time she had ever had public prayer.

J.B. ,Dalles, OR, USA

 

Testimony 8

Thank you for the ministry you are sharing with us, it is a real blessing to us and especially to my husband and myself! You are encouraging us to think for ourselves and not just to except everything, without thinking it through, with God’s word!

M.K., USA

 

Testimony 53

I was so blessed by a friend who gave me your book, “The God Shaped Brain,” while I was sitting in church asking God to please help me learn more about Him and help me not to be so confused and scared. That was about 2 years ago. Your books have helped me to love God even more. I’m not confused or scared anymore! I have listened to all of your bible study classes and feel like I know the wonderful people that attend every week. Thank you for all that you’re doing in spreading the true message about God and His law of love. God bless you and your whole class.

Elssy P., Modesto, CA, USA

 

Testimony 2

I continue to enjoy your lessons every week. The more that I research your conclusions, the more I am convinced that the Holy Spirit has lead you to distill out the essence of human redemption. Thank you for your courageous stand for the truth.

S. G., TX, USA

 

Testimony 61

I grew up in a prominent protestant church and had what I like to call religious anxiety. I’ve always had questions about God and Salvation that no one could seem to answer.  I didn’t know how to find resolution. During 2020, at the height of my anxiety, I fell to my knees and begged God to show me truth and light and to give me the hope that I’ve been longing for. Days later, I stumbled upon your online videos and it was like a veil was lifted and EVERYTHING made sense! For the first time in my almost 39 years of life, my religious/spiritual anxiety has lessened. I feel a sense of freedom and peace I’ve NEVER had before… and it’s all because my view of God has changed. Thank you!

Ashleighn C.