Call Us: 423 661-4734 | Email: requests@comeandreason.com      
WATU WA NDANI, WATU WA NJE, NA MPANGO WA MUNGU KWA MAISHA

WATU WA NDANI, WATU WA NJE, NA MPANGO WA MUNGU KWA MAISHA

Hivi karibuni, msikilizaji mmoja mtandaoni alituma maswali yafuatayo:

Je, watu huwa aidha watu wa ndani au watu wa nje? Je, wewe ni mmoja kati ya hao? Yesu alikuwa nani kati ya hao? Je, unaweza kuwahudumia watu ikiwa wewe ni mtu wa ndani?

Katika miaka ya 1920, daktari wa akili Carl Jung alibuni maneno mtu wa ndani(introvert) na mtu wa nje (extrovert) ili kuelezea aina mbili za tabia. Mtu wa ndani hulenga nguvu zake za kiakili na hutegemea nafsi yake ili kujipatia upya na kujichangamsha, ilhali mtu wa nje hulenga nguvu zake nje na hupata hali ya kujipatia upya na kujichangamsha kupitia wengine.

Tangu wakati huo, mengi yameandikwa kuhusu mitindo hii miwili ya tabia, na aina zake ndogo nyingi pia zimeelezewa. Nadharia zimependekezwa kuhusu tofauti katika kazi za mizunguko ya ubongo, uzoefu wa maisha, mifumo ya mtiririko wa damu, kemia ya neva, vinasaba, na majibu yanayojifunzwa, lakini hakuna maelezo ya kibaolojia yaliyo kubalika kwa wote ambayo yamepatikana.

Lakini katika kutafuta ufahamu, muulizaji kwa hekima alimrejelea Yesu. Alijiuliza: Yesu alikuwa mtu wa ndani au mtu wa nje?

Yesu alikuwa mwanadamu mkamilifu na pia alikuwa udhihirisho wa Mungu. “Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake” (2 Wakorintho 5:19). Yesu alisema, “Mtu yeyote aliyeniona mimi amemwona Baba” (Yohana 14:9). Na Yesu ndiye Mungu aliyefanyika mwanadamu (Yohana 1:1–3, 14).

Yesu ni Mungu katika ubinadamu, na ndani ya Yesu tunaona utekelezaji, uhai, na dhihirisho la tabia ya Mungu ya upendo na ukweli. Upendo wa Yesu ulimfanya azingatie wengine, katika kuokoa, kuponya, kubariki, kuinua, na kumpea Baba yake utukufu. Hivyo basi, wakati upendo na ukweli vilipohitaji, Yesu alikuwa mtu wa nje katika kupeleka mbele ukweli na upendo (uponyaji wa hadhara, mahubiri, miujiza ya kuwalisha maelfu, n.k.); lakini wakati upendo na ukweli vilipomhitaji, Yesu alikuwa mtu wa ndani (kunyamaza, kuondoka kimya kimya, n.k.).

Yesu hakuwa mtu wa ndani kwa mujibu wa ufafanuzi wa Jung wa kujielekeza ndani ya nafsi yake ili kupata nguvu na kujichangamsha, wala hakujitenda kama mtu asiyeonekana. Vilevile hakuwa mtu wa nje kwa kutafuta nguvu na kujichangamsha kutoka kwa watu, wala hakujionyesha kama mtu wa sherehe anayependa kuwa kitovu cha furaha.

Badala yake, Yesu alikuwa dhihirisho kamili la mpango wa Mungu kwa ajili ya binadamu. Alitafuta nguvu na kujichangamsha kwa kuwa na muda na Baba yake, akimpenda Baba yake kwa moyo wake wote, akili zake zote, nafsi yake yote, na nguvu zake zote. Alijitenga na watu kwa muda ili kupata nguvu na kujichangamsha pamoja na Baba yake, kisha akatoka kuwahudumia wengine kwa ukweli na upendo wa Mungu, akitenda kama mtu wa nje katika hali zilizosaidia kuendeleza ufalme wa Mungu na akitenda kama mtu wa ndani katika hali zilizosaidia kuendeleza ufalme wa Mungu.

Yesu alikuwa udhihirisho wa upendo na ukweli uliomtukuza Baba na kuwabariki watu.

Katika ulimwengu huu wa dhambi, roho ya hofu na ubinafsi iliyo ndani ya mwanadamu humfanya atafute amani na faraja—kile kinachomfanya ajihisi salama zaidi. Watu wa ndani na watu wa nje, kama Jung alivyowafafanua, mara nyingi ni watu wasio na usalama wa ndani wanaojaribu kufidia hofu zao za ndani—hofu ya kukataliwa, upweke, kutotosheleza, hatia, na aibu—kupitia sura yao ya kuwa mtu wa ndani au wa nje.

Kwa maneno mengine, introvert anaweza kuwa anajitegemea kupita kiasi anaposhughulika na wengine, akachoka na kuchoshwa, kisha ajitenge ili kujichaji upya; au hujitenga ili kuepuka wasiwasi unaotokana na hofu ya kutotosheleza, hofu ya kufanya makosa, hofu ya watu watasemaje, aibu, n.k., na hivyo hujiondoa ili kuepuka umakini juu yake. Extrovert, kwa kuwa mchangamfu, mwenye sauti kubwa, mcheshi, na mwenye kuburudisha, mara nyingi hufanya hivyo akitafuta kukubalika na sifa kutoka kwa wengine ili kufidia hofu na kutokujiamini vilivyo ndani yake.

Yesu anawaita wote— introvert na extrovert—wamgeukie Yeye wawe conVERTS! Yesu anawasihi wote waache maisha ya hofu na ubinafsi tuliyorithi kutoka kwa Adamu, na wazaliwe upya wakiwa na roho mpya na moyo mpya, wakiwa na Roho wake wa upendo na uaminifu, na wasiishi tena wakitawaliwa na roho ya hofu. Na mioyo yetu ikizaliwa upya kwa roho ya upendo na uaminifu, hatutafuti tena nguvu kutoka kwetu wenyewe au kutoka kwa watu, bali kama Yesu, kila siku tunatumia muda pamoja na Yeye na Baba yetu wa mbinguni na kupata nguvu, uhai, msukumo, na motisha kutoka kwake. Kama Biblia inavyosema, upendo wa Kristo unatuchochea (2 Wakorintho 5:14).

Kwa moyo huu mpya wa upendo, na akili zetu zikiwa zimemwelekea Yesu badala ya nafsi zetu, tunatafuta kumtukuza Mungu kwa kutimiza makusudi yake katika maisha yetu. Kwa hiyo, tutatenda kwa namna ya mtu wa nje pale ambapo hilo linamtukuza Mungu na kuwabariki wengine, na tutatenda kwa namna ya mtu wa ndani pale tunapohitaji kunyamaza na hilo linamtukuza Mungu. Lakini msukumo wetu wa ndani hautakuwa tena hofu na kutokujiamini, bali upendo na uaminifu kwa Mungu—kwa utukufu wake na baraka ya wengine.

Hatimaye, usichanganye utu wa ndani na utu wa nje na vipawa—watu wengine wamepewa kipawa cha muziki, cha kuzungumza, na cha uongozi ambacho kitawaita katika majukumu yanayoonekana kwa namna ya “watu wa nje.” Wengine watapewa uwezo na talanta zinazofanya kazi kwa ufanisi zaidi nyuma ya pazia na kuonekana kama “watu wa ndani.” Lakini mtu ambaye si wa ndani wala wa nje, ambaye ni kama Yesu, atajikuta akifuata uongozi wa Roho Mtakatifu, na wakati hali ni kwamba ufalme wa Mungu unasonga mbele kwa ufanisi zaidi kupitia kimya, msemaji, mwanamuziki, au kiongozi atabaki kimya, au kama Yesu, ataondoka kimya kimya. Na wakati hali ni kwamba ufalme wa Mungu unasonga mbele kwa ufanisi zaidi, mtu ambaye kwa kawaida hutimiza majukumu yake nyuma ya pazia atasema kwa ujasiri akifuata msukumo wa Roho Mtakatifu.

 

 

 

Donate online, securely via PayPal using your credit or debit card (no PayPal account needed, unless you want to set up a monthly, recurring payment).


cancel recurring payment

 

Want to use zelle instead?
See how on our
Support and Donations page.

Upcoming Events

calendar

Testimonial Post Slider

Testimony 38

Since November 2015, when I started studying Gods word from this God Is Love point of view, my life has been transformed. My troubled marriage of 15 years has been healed and my husband and I are truly happy for the first time in 15 years. Now When I read the word of God I understand it so much better and I can’t help but see Gods love radiating through the pages to humanity. Gods word is living and active and I am blessed beyond measure to be having this amazing experience. God has given me a beautiful understanding of Jn 3:16 that amazes me more and more each day. Thank you again for your ministry.

Helen D., London, England

 

Testimony 9

I really enjoy with you the view of a gracious God. Thank you for sharing the work you are allowing the Lord to do in you.

L., Queensland, Australia

 

Testimony 35

I am so pleased with the response your message is receiving at my church from the middle-aged to the young adults. I have given out 100 copies of the first two seminars and there are more request every week. One of my [class members] came to me after viewing the series, grateful and impressed with how easy the message was retained. He had been a Seventh-day Adventist in fear all his life, and felt like the scales were removed from his eyes after viewing the seminars. I am so impressed by the change I see in members who have received this message, we are in one accord. However, I am sadden by the negative response of the older people. I am verbally attacked anytime I talk about imposed laws, but I believe my mission is to enlightened everyone I can. I watch your Bible Study Class on YouTube every Friday night and I feel like I am apart of the class. All of you are in one accord and I am so blessed to have found you. I pray that all of you continue to spread this message and I am committed to doing my part.

Clara S., Westfield, MA, USA

 

Testimony 34

I was introduced to Come and Reason Ministries by accident, via a passing comment made in a bible study class we were visiting. I checked this website out and my life was changed. The understanding of the truth of God’s character, and how we apply it, is so right. The tricky part is consistently applying which “lens” to look through. As I began to understand, I started sharing the basics of this understanding with a discussion group I was leading and, suddenly, a lot of things started to make sense that never used to. At the same time, I enjoyed an amazing opportunity. I was able to conduct a full bible study at WORK! What an amazing experience! It is such a joy to share the truth about God and to share how it all fits in the war between God and Satan. So many people benefit when we have a correct understanding about how God works and who He really is! Thank you for this transformational understanding. Keep up the good work! God Bless you!

Tony P., CA, USA

 

Testimony 36

Thank you and may God continue to bless you as you share with others the intricacies of how we are all “fearfully and wonderfully made”. I must share that you have opened a whole new world to me, and I have found tremendous healing through what you have shared in two of your books, “Could It Be This Simple?” and “The God Shaped Brain.” I praise God for what you shared, what I have learned, and how I have grown and healed! My prayer is that My Precious Jesus will be seen by others in the way I live, act, talk, etc. and they may be encouraged to know He is truly a GREAT God of LOVE, desiring that no one should perish! God Bless you in your continued endeavors to present Him as He really is!

Joleen H. GA, USA

 

Testimony 59

I’m a native Ghanan, but am currently in France for my master’s degree. Prior to this, during my final years at undergraduate studies in Ghana, I was introduced to your ministry and I’ve been immensely blessed by what you share, especially about the Design and Imposed Laws. God richly bless you for that.

One of the first things I did when I arrived in France was to buy all four of your books. They not only helped me, but those I shared them with. I shared the message with an atheist student and I marveled at how God worked mightily in his life. Today this person shares the Love of God with others and debunks theories of who God is not. I want to share what you present in your “Heavenly Sanctuary and Investigative Judgment” pamphlet, because the message brought rest to my soul and I live today as a healthy person.

God bless you so much and your ministry.

Michael A., Ghana

 

Testimony 65

I have been tuning into your weekly study classes for a while now and wanted express my appreciation for the teachings that ha been a huge blessing in opening up the true message of the word. Viewing scripture under an imposed law theory always, without fail, raised more questions, concerns, and conflicting scripture interpretations that were discouraging at the very least. Looking at scripture through the design law lens has brought more truth to light for me personally and an understanding of our Heavenly Father that places Him “above all others,” where I am now more than thrilled to witness and serve Him.  I “stumbled” across this ministry a year or so ago and would only watch a few minutes at a time. But the more I listened and the longer I paid attention, the more my spiritual eyes were opened to the ever present truths of scripture. The comprehension of the great controversy and it’s origin by the lies perpetrated and perpetuated throughout the Bible on the attack of God’s character and government is truly priceless. Keep up the Good Work! Your servanthood is desperately needed in such a time as this!

Jeff D., Reading, MA, USA

 

Testimony 2

I continue to enjoy your lessons every week. The more that I research your conclusions, the more I am convinced that the Holy Spirit has lead you to distill out the essence of human redemption. Thank you for your courageous stand for the truth.

S. G., TX, USA

 

Testimony 42

I am just writing to say that I have been so blessed by the teachings of Come And Reason Minitries recently. I watched last week’s bible study lesson on Youtube and am thankful that the error in the printed lesson guide you use was pointed out and this week’s study was of equal benefit, if not more so. My understanding of God’s nature has been very confused of late and I am so grateful for clarity in this matter. I have never really fully understood previously how a good God can cause bad things to happen and now I realise that He doesn’t, it’s a natural consequence of sin. May the almighty Father and His Son, our Saviour Jesus Christ, continue to bless your ministry.

Laura P., United Kingdom

 

Testimony 16

Your seminars are still inspiring and changing our lives and we continue to share the principles we have learned from you. Your ministry has changed our lives!

E.W.

 

Testimony 69

After reading your book, ‘Could It Be This Simple,’ someone was explaining Christianity in a way that made sense to me for the first time in my life. One morning, I simply prayed “I’m sorry and I love you.” As soon as I silently said that, I could literally feel God’s presence and light flood down on me from above and fill me up with love and joy. I sat there crying my eyes out, because I was so overpowered with this feeling of love and joy. It was just so incredible. I hope that more people can read this book and get a blessing from it. It’s really amazing.

Rachael H.

Testimony 48

I just want to tell you how blessed I have been reading “The Remedy!” It has become a daily part of my devotional relationship with God. In it I have found a God of love and a God that loves me! The bible has come alive for me! It is the first time that I can say that I have felt hope fill my heart as I have read God’s word. This is good news I can share! Thank you, Dr Jennings! Thank you for your heart for others. I can’t put into words how this has set me free! It has strengthened my trust and love for God.

Jason H.

 

Testimony 5

We listen to your bible studies lessons in our class in Montana. You actually were the main reason I decided to get a laptop, so I can go to your site and listen, read, learn, and print the class notes. I am so grateful to learn the correct view of God and his character. Now, to just have others have an interest in knowing, so I can share it with them. Good thoughts your way.

R. N., MT, USA

 

Testimony 61

I grew up in a prominent protestant church and had what I like to call religious anxiety. I’ve always had questions about God and Salvation that no one could seem to answer.  I didn’t know how to find resolution. During 2020, at the height of my anxiety, I fell to my knees and begged God to show me truth and light and to give me the hope that I’ve been longing for. Days later, I stumbled upon your online videos and it was like a veil was lifted and EVERYTHING made sense! For the first time in my almost 39 years of life, my religious/spiritual anxiety has lessened. I feel a sense of freedom and peace I’ve NEVER had before… and it’s all because my view of God has changed. Thank you!

Ashleighn C.

 

Testimony 50

After coming into contact with Come And Reason Ministries, I can finally say that many of my unanswered questions have fallen into place. I discovered that my view of God’s Law was “imposed laws and rules” with “imposed punishments” and that this was the major culprit of my many unanswered questions. Thanks be to God for using you and those around you to help us who have struggled with this “infection” of thought. I have now rejected the “imposed law” concept to fully embrace “Design Law”… to look thru “Design Law,” instead of “imposed law,” is a relief.

Viliami L., Australia