Call Us: 423 661-4734 | Email: requests@comeandreason.com      
KAMA UNGEKUWA MYAHUDI MWAMINIFU MIAKA 2,000 ILIYOPITA

KAMA UNGEKUWA MYAHUDI MWAMINIFU MIAKA 2,000 ILIYOPITA

Kama ungekuwa Myahudi mwaminifu mwaka wa AD 27, ungekua umeamini nini? Ungekuwa unamwamini nani? Ungeweka uaminifu wako wapi?

Maisha yako yote, ungekuwaumefundishwa na wazazi wako, walimu, na makuhani kwamba wewe uu sehemu ya watu maalum waliochaguliwa na Mungu, watu walio na maandiko yaliyovuviwa na manabii na walio kuwa wakingoja ujio wa Masihi.

Maisha yako yote, ulifundishwa kwamba dini zote zingine duniani zilikuwa za uongo.

Maisha yako yote, umekuwa ukishiriki Sabato kila wiki, kutoa dhabihu hekaluni mara kwa mara, na kusherehekea sikukuu za kila mwaka kama vile Pasaka na Siku ya Upatanisho (Yom Kippur).

Maisha yako yote, umekuwa ukiwaamini viongozi wa dini—makuhani, baraza la Sanhedrin—kufafanua maandiko matakatifu, kukuambia wajibu wako kwa Mungu, kueleza kilicho sahihi au kibaya kwa dini, na kubaini uzushi na kukufuru.

Na maisha yako yote yangekuwa mzigo—maisha chini ya hofu ya dhambi, uzito wa masharti ya dini, hofu ya kushindwa, shaka isiyokoma, hisia ya kutofaa, wasiwasi wa kudumu kwamba labda licha ya kulipa zaka zako zote, kutoa dhabihu zote, na jitihada zako zote za kufuata kanuni, bado hukukubalika na Mungu.

Kama ungekuwa Myahudi huyo, ungefanya nini? Je, kulikuwa na taasisi nyingine ya kidini ambayo Mungu alikuwa akiitumia zaidi ya Israeli? Kulikuwa na Biblia bora zaidi yenye ufunuo sahihi zaidi kuliko Torati?

Je, hilo lingemaanisha kwamba uongozi wa taasisi ya Kiyahudi ulikuwa unafundisha ukweli?

Ikiwa ungekuwa Myahudi miaka 2000 iliyopita, ingekuwa busara kuwatumainia makuhani, Walawi na Sanhedrini kuamua ni nini kilicho kweli? Nini mapenzi ya Mungu? Dhambi ni nini? Mtu anaokokaje kutoka katika dhambi?

Viongozi wa dini wa Kiyahudi walikosea wapi? Walifunika tafsiri zao za Maandiko kwa ufahamu usio sahihi wa sheria. Waliona sheria ya Mungu ikifanya kazi kama sheria za kibinadamu—kanuni zilizowekwa ambazo zinahitaji adhabu za kubuni. Kwa hivyo walipotosha ibada na mifano kuwa masharti ya moja kwa moja ya wokovu, badala ya maonyesho, mfano na somo la kivitendo lililokusudiwa kufundisha ukweli.

Kisha Yesu akaja na akafundisha kwa mamlaka—mamlaka ya jinsi uhalisia unavyofanya kazi. Hadithi Zake zote ziliwafundisha watu kwamba sheria za Mungu ni sheria za mpangilio wa uumbaji—kanuni za jinsi maisha yanavyofanya kazi. Yesu alivunja sheria za dini zilizowekwa na wanadamu ili kuendeleza ufalme wa mbinguni. Yesu aliponya siku ya Sabato na kula na makahaba, watoza ushuru, na Wasamaria. Kwa nini? Kwa sababu Yesu hushughulika na uhalisia—na uhalisia ni kwamba Mungu aliumba wanadamu kama jamii moja Edeni. Adamu alijipata katika hali ya dhambi, hivyo kila mwanadamu huzaliwa katika hali hiyo ya dhambi (Zaburi 51:5); kila mtu anahitaji tiba ile ile ya shida hii; na Yesu alikuja kuondoa dhambi ya ulimwengu (Yohana 1:29) ili kutoa tiba ya hali yetu ya dhambi, kuwaokoa na kuwaponya wote wanaoshiriki kile alichotoa (Wagalatia 2:20; 2 Petro 1:4). Dhambi haiwezi kutatuliwa kwa sheria na kufuata sheria—bali kwa uumbaji upya, uponyaji, usafishaji wa moyo na akili kwa nguvu ya uumbaji wa Mungu!

Yesu alisema,

“Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu kiasi cha kumtoa Mwanae pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwanae kuuhukumu ulimwengu bali auokoe.” (Yohana 3:16,17).

“Njooni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jifungeni nira yangu; jifunzeni kutoka kwangu; kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. Kwa maana nira yangu ni rahisi, na mzigo wangu ni mwepesi.” ( Mathayo 11:28 -30

Na viongozi wa dini—viongozi wa watu wa Mungu walioteuliwa—walipomwona Yesu akiponya, kubariki, na kusamehe, walisema:

“Je, sisi hatusemi kwa haki ya kuwa wewe ni Msamaria na una pepo?” (Yohana 8:48).

Kama ungekuwa Myahudi mwaminifu miaka 2,000 iliyopita ukifanya kazi kwa ajili ya “kanisa,” ungejibuje?  kama viongozi wako wangekuuliza maswali haya kama walivyouliza wafuasi wao:

Hatimaye wale walinzi wa Hekalu waliokuwa wametumwa kum kamata Yesu, walirudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo. Wakauli zwa, “Mbona hamkumleta ?”

Wale walinzi wakajibu, “Hakuna mtu ambaye amewahi kufundisha kama yeye.”

Mafarisayo wakajibu, “Ameweza kuwa danganya hata ninyi? Je, mmewahi kuona kiongozi ye yote au mmoja wa Mafarisayo ambaye amemwamini? Lakini huu umati wa watu wasiojua sheria ya Musa, wamelaaniwa.”  (Yohana 7:45–49).

Kwa hiyo, kama ungekuwa Myahudi mwaminifu miaka 2,000 iliyopita, ungeendelea kuwa mwaminifu kwa kushikamana na dhehebu lako, mafundisho ya walimu, makuhani, Walawi, na Sanhedrin? Au kama ungelifuata viongozi hao wa mfumo wa Mungu uliobarikiwa, ungegeuka kutoka uaminifu kwenda uasi na kujiunga nao katika kumsulubisha Yesu?

Na leo je?

Kama wewe ni Mkristo mwaminifu, unayehusishwa na dhehebu linalodaiwa kuitwa na Mungu kupeleka injili kwa ulimwengu na kuendeleza mafundisho “sahihi,” je, utaweza kubaki mwaminifu kama ukiwaachia wachungaji, makasisi, maprofesa wa theolojia, na viongozi wa kanisa wafikirie badala yako—au sharti ufikirie mwenyewe na ujue ukweli mwenyewe?

Kama Paulo alivyoshauri katika Warumi 14:5, je, hautakiwi kushawishika kabisa katika akili yako kuhusu kilicho kweli? Inawezekana kwamba ili kubaki mwaminifu kwa Yesu, itakulazimu kuwa kama Petro, Paulo, na mitume wengine—na kukataa mafundisho ya viongozi wa kanisa lako?

Haya si mambo ya kubuni—ni historia. Yametokea tena na tena. Kama mwanzilishi mmoja wa Kanisa la Waadventista alivyoandika katika Tumaini La Vizazi Vyote:

“Sanhedrini walikuwa wameukataa ujumbe wa Kristo na walikuwa wameazimia kumuua; kwa hiyo Yesu aliondoka Yerusalemu, kutoka kwa makuhani, hekalu, viongozi wa dini, watu waliokuwa wamefundishwa katika sheria, na akageukia kundi jingine ili kulitangazia ujumbe Wake, na kuwakusanya wale ambao wangeibeba injili kwa mataifa yote.

Kama vile nuru na uzima wa wanadamu vilivyokataliwa na viongozi wa kidini katika siku za Kristo, ndivyo vilivyokataliwa katika kila kizazi kilichofuata. Mara kwa mara historia ya Kristo kujitenga na Uyahudi imerudiwa. Wakati Wanamatengenezo walipohubiri neno la Mungu, hawakuwa na wazo la kujitenga na kanisa lililoanzishwa; lakini viongozi wa kidini hawakuvumilia nuru hiyo, na wale waliokuwa wakiibeba walilazimishwa kutafuta kundi jingine lililokuwa likitamani ukweli. Katika siku zetu wachache miongoni mwa wanaodai kuwa wafuasi wa Wanamatengenezo wanaongozwa na roho yao. Wachache wanasikiliza sauti ya Mungu na wako tayari kukubali ukweli katika sura yoyote utakayowasilishwa. Mara nyingi wale wanaofuata nyayo za Wanamatengenezo hulazimika kugeuka kutoka kwa makanisa wanayoyapenda ili watangaze mafundisho ya wazi ya neno la Mungu. Na mara nyingi wale wanaotafuta nuru hulazimishwa na mafundisho hayo hayo kuyaacha makanisa ya baba zao ili waweze kutii.

Ninakutia moyo: Usije ukaanguka katika mtego wa kusalimisha  akili yako kwa wengine; daima fikiria mwenyewe na ubaki mwaminifu kwa Yesu kuliko mtu yeyote mwingine.

 

 

Donate online, securely via PayPal using your credit or debit card (no PayPal account needed, unless you want to set up a monthly, recurring payment).


cancel recurring payment

 

Want to use zelle instead?
See how on our
Support and Donations page.

Upcoming Events

calendar

Testimonial Post Slider

Testimony 69

After reading your book, ‘Could It Be This Simple,’ someone was explaining Christianity in a way that made sense to me for the first time in my life. One morning, I simply prayed “I’m sorry and I love you.” As soon as I silently said that, I could literally feel God’s presence and light flood down on me from above and fill me up with love and joy. I sat there crying my eyes out, because I was so overpowered with this feeling of love and joy. It was just so incredible. I hope that more people can read this book and get a blessing from it. It’s really amazing.

Rachael H.

Testimony 31

It was very touching to hear the testimony of your class share how viewing God’s true character has changed their lives. My feelings are the same – there is so much freedom in knowing that God LOVES me – regardless of my… just, REGARDLESS! I’m still blown away by the true gospel, the fact that God is not ready to strike us when we fail. He is not arbitrary. He simply loves us and warns of the natural consequences because He can’t stand to see us suffer. I AM IN LOVE WITH THIS GOD!!!

Ceil V.,  UT, USA

 

Testimony 35

I am so pleased with the response your message is receiving at my church from the middle-aged to the young adults. I have given out 100 copies of the first two seminars and there are more request every week. One of my [class members] came to me after viewing the series, grateful and impressed with how easy the message was retained. He had been a Seventh-day Adventist in fear all his life, and felt like the scales were removed from his eyes after viewing the seminars. I am so impressed by the change I see in members who have received this message, we are in one accord. However, I am sadden by the negative response of the older people. I am verbally attacked anytime I talk about imposed laws, but I believe my mission is to enlightened everyone I can. I watch your Bible Study Class on YouTube every Friday night and I feel like I am apart of the class. All of you are in one accord and I am so blessed to have found you. I pray that all of you continue to spread this message and I am committed to doing my part.

Clara S., Westfield, MA, USA

 

Testimony 9

I really enjoy with you the view of a gracious God. Thank you for sharing the work you are allowing the Lord to do in you.

L., Queensland, Australia

 

Testimony 74

Thank you so much for opening my eyes. I’ve been through a lot of ministries that just didn’t show the love of God that I felt he was. You have helped me to begin the process of true healing. I thought I was “too far gone,” now I know there’s hope in Jesus, because he loves us beyond what we can comprehend. Thank you again for all you do. I truly appreciate it and pray more people find you (physical at your studio and through this website).

Dalio M.

Testimony 5

We listen to your bible studies lessons in our class in Montana. You actually were the main reason I decided to get a laptop, so I can go to your site and listen, read, learn, and print the class notes. I am so grateful to learn the correct view of God and his character. Now, to just have others have an interest in knowing, so I can share it with them. Good thoughts your way.

R. N., MT, USA

 

Testimony 73

I have been truly blessed by your blogs and other resources. They have helped me to see things in a much brighter light and to reason things out better. Thank you so much for your ministry. Whenever I have the opportunity I pass along your material to my friends.

R. Noseworthy, Newfoundland, Canada

Testimony 75

Thank you so much for everything you do! Because of all these truths, I’m excited to be with Jesus! I always pray everyday, “COME TODAY, JESUS.” Before finding C&R, I was always praying for delays, “NOT TODAY OH GOD. I AM NOT READY.” I just need to share more, talk more bout this truth, so everybody will be excited for Jesus.

J C Shin

Testimony 23

I would just like to add my voice to the many people who, I believe, must have contacted you to express their appreciation for the “Healing the Mind” DVDs. I’ve been listening to your Bible study class discussions for many years and I’ve been personally blessed by your research and teaching about the character of God.

L. G., Oakland, MI, USA

 

Testimony 20

I just wanted to personally thank you for your teachings and insight into scripture. I came across your website via my cousin who suggested I look into “Healing the Mind” information. My youngest daughter has been struggling over the last couple of years and it all came to a head this spring. When I started listening to the “Healing the Mind” lectures my own life began to be transformed. I began sharing with all my daughters the concepts you laid out so clearly. I ordered your book and soaked it up. I just want to say “Thank You!” My walk with the Lord has been refreshed and renewed. Your obedience to the Lord is a blessing to so many.

R. K., Anderson, SC, USA

 

Testimony 65

I have been tuning into your weekly study classes for a while now and wanted express my appreciation for the teachings that ha been a huge blessing in opening up the true message of the word. Viewing scripture under an imposed law theory always, without fail, raised more questions, concerns, and conflicting scripture interpretations that were discouraging at the very least. Looking at scripture through the design law lens has brought more truth to light for me personally and an understanding of our Heavenly Father that places Him “above all others,” where I am now more than thrilled to witness and serve Him.  I “stumbled” across this ministry a year or so ago and would only watch a few minutes at a time. But the more I listened and the longer I paid attention, the more my spiritual eyes were opened to the ever present truths of scripture. The comprehension of the great controversy and it’s origin by the lies perpetrated and perpetuated throughout the Bible on the attack of God’s character and government is truly priceless. Keep up the Good Work! Your servanthood is desperately needed in such a time as this!

Jeff D., Reading, MA, USA

 

Testimony 13

I borrowed “Healing The Mind” DVDs from a friend and showed them at my home for a small gathering of women friends. Neither of my friends are Adventist, but they both enjoyed and embraced the messages you taught. In fact, one of the ladies prayed out loud in our group and that was the first time she had ever had public prayer.

J.B. ,Dalles, OR, USA

 

Testimony 3

My husband is a pastor and I listen to your lesson almost every week. Thank you for helping me in my study life and to help me love the “real” God more.

C. F., NC, USA

 

Testimony 57

You have helped make sense of thirty two years of confusion. The material you freely provide reorganized so much of my life into such a beautiful pattern that has always been hinted at from within, but misguided with my training and what I was experiencing externally. My filipno parents, who were converted from Catholicism to SDA, were sincere and did their best to raise me the right way and I have deep respect for them. However, being immigrants and not understanding the language made for a difficult transition as I was growing up, which also applied to my spiritual growth as I learned the patterns of religion. I have been listening to as many bible study classes and reading blog posts as my time in a work truck will allow, searching for the practical applications of where spirituality and reality meet, and I thank you for helping me find that. You have helped me reach a point in which I can truly say that I love God, that I believe He loves me, and, like David, I delight in His law. God bless.

Emmanuel V., Calgary, AB Canada

Testimony 64

I’ve been reading the bible and walking with Jesus since I was around 16. I’m 42 now. I’ve mostly been alone in my walk although I went to several churches in different denominations. For the past 3 years God has been showing me His character of agape. It’s been a blessing and changed how I view God and my walk with Jesus. About a year ago I came across the power of love and the principles of design law. These teachings changed how I read scripture and have been such a beautiful blessing. I’m very excited and grateful for these truths. We share these truths of agape, design law and the reality of the principles of the two trees in the garden of Eden with people on Facebook and YouTube. People all over are learning to trust God and His agape design law which makes life possible. Thank you for everything you shared with me. May God continue to bless your ministry and lives.

Bradley M., Hinsdale, NY, USA